Afariki kwa kuchomwa kisu kisa Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu

Mabishano ya  ushabiki wa  Yanga na Simba yamesababisha kifo cha mwanaume mmoja aliyefahamika  kwa jina la Evaristo Mwambogolo (28), mkulima na mkazi wa Ululu wilayani Mbozi mkoani Songwe, baada ya kuchomwa kisu kifuani na mtu aliyejulikana kama Exavery Mwaweza.

Taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi mkoani humo, imesema Mwambogolo alifariki dunia akiwa njiani wakati akikimbizwa Zahanati ya Iyula kwa ajili ya matibabu.

“Uchunguzi wa awali umeonesha chanzo cha tukio hilo ni ushabiki wa mpira wa timu ya Simba na Yanga kati ya marehemu na mtuhumiwa, ambapo mtuhumiwa alitumia kisu alichokuwa nacho wakati wa ugomvi huo, mara baada ya kutenda kosa hilo, alitoroka kusikojulikana, ” imesema taarifa hiyo.

Aidha, Jeshi hilo limesema linafanya msako mkali wa kumtafuta mtuhumiwa huyo ili akamatwe na aweze kuhukumiwa kwa mujibu wa sheria.

spot_img

Latest articles

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

Serikali yaahidi kuimarisha uwezeshaji wa Makundi Maalum kupitia ajenda ya Maendeleo Jumuishi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt....

More like this

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...