Media Brains,AGRA zapongezwa kwa kuwanoa wanahabari kuhusu mbegu bora

Na Winfrida Mtoi, Media Brains

MWENYEKITI wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile, amezipongeza kampuni ya Media Brains na Shirika linalojihusisha na Kuendeleza Mifumo ya Chakula Afrika (AGRA) kwa kuandaa mafunzo kwa wanahabari yanayohusu mbegu bora za kilimo na mfumo wake wa uzalishaji.

Media Brains na AGRA zimeandaa mafunzo hayo ya siku mbili yaliyofanyika Novemba 3-4, 2023 katika hoteli ya Oceanic iliyopo Bagamoyo, yakihusisha wahariri wa vyombo vya habari na waandishi wa habari.

Balile ambaye ni kati ya washiriki, amesema mafunzo hayo ni ya kipekee ambayo ni tofauti na waliyozoea kufanya mengi yakilenga zaidi masuala ya siasa.

Dr. Emmarold Mneney akitoa mada kwa wahariri na waandishi wa habari wakati wa mafunzo hayo.

“Niwapongeze Media Brains na AGRA kwa kuandaa mafunzo haya ya kipeke, mikutano kama hii inayogusa wananchi moja kwa moja imekuwa haipewi kipaombele,” amesema Balile.

Wawezeshaji katika mafunzo hayo ni watafiti wabobezi katika masuala ya mbegu kutoka taasisi mbalimbali, akiwamo Dk. Emmarold Mneney ambaye amebainisha kuwa mbegu bora ina uwezo wa kukabiliana na tabianchi.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Media Brains, Jesse Kwayu akitoa neno katika mafunzo hayo.

Dk. Mneney amefafanua kuwa mabadiliko ya tabianchi hayawezi kukwepeka na njia ya kukabiliana nayo ni kuzalisha mbegu zilizoboreshwa ili kufikia lengo la kuilisha dunia.

“Elimu ya mbegu haipo ya kutosha, inatakiwa kutolewa kwa vitendo ili wananchi waweze kuhamasika na kuzalisha mbegu zenye ubora,” ameeleza Dk. Mneney.

Naye Dk. Geradine Mzena kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania TARI, amesema kutokana na ongezeko la idadi ya watu na wazalishaji wa mbegu wanatakiwa kuwa wengi ili kupata chakula kinachotosheleza.

“Ni kweli mbegu hazitoshi lakini Serikali imeanza kujenga maeneo mengine ya kuzalisha mbegu ili kulinda chakula,” amesema.

spot_img

Latest articles

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora yaweka wazi nafasi yake kwenye Uchaguzi Mkuu

Na Tatu Mohamed TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imesema kuwa ina...

TMDA yaendelea kuelimisha umma juu ya matumizi sahihi ya dawa Sabasaba

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Imeendelea kutoa Elimu kwa...

Mazingira wezeshi ya Serikali yafungua fursa mpya za Uwekezaji kupitia TAWA

📍 Milango ya uwekezaji bado iko wazi Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usimamizi wa...

CRDB yamkabidhi Rahabu Mwambene zawadi ya gari aina ya Ford Ranger XLT 

Na Mwandishi Wetu  BENKI ya CRDB imemkabidhi Rahabu Mwambene zawadi ya gari aina ya Ford...

More like this

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora yaweka wazi nafasi yake kwenye Uchaguzi Mkuu

Na Tatu Mohamed TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imesema kuwa ina...

TMDA yaendelea kuelimisha umma juu ya matumizi sahihi ya dawa Sabasaba

Na Tatu Mohamed MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA), Imeendelea kutoa Elimu kwa...

Mazingira wezeshi ya Serikali yafungua fursa mpya za Uwekezaji kupitia TAWA

📍 Milango ya uwekezaji bado iko wazi Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usimamizi wa...