TRA yawaalika wananchi Sabasaba kupata elimu ya Kodi na huduma za TIN

Na Tatu Mohamed

MAMLAKA ya Mapato nchini (TRA) imewaita wananchi kutembea banda lao lililopo katika Viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) maarufu kama Sabasaba ili kupata elimu na huduma mbalimbali za kikodi.

Akizungumza na waandishi wa habari katika banda lao lililopo katika Viwanja vya Maonesho hayo ambayo ni ya 49, Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipa Kodi na Mawasiliano wa TRA, Richard Kayombo amesema wameshiriki katika Maonesho hayo kwa ajili ya kuendeleza kutoa elimu ya kodi kwa wadau wanaofika katika viwanja hivyo.

Amefafanua kuwa katika maonesho hayo TRA ina mambo mengi ikiwemo kuwaelekeza watu kuagiza bidhaa pamoja kuwaelekeza bidhaa zenye misamaha ya kodi.

“Tumeona tuje ili kuwaelimsiha wadau mambo mapya na ya zamani kuhusu Chuo cha kodi, vivutio vya kodi, sekta za kilimo pia ukija bandani kwetu utapata huduma ya kupata TIN namba hapa hapa bandani,” amesema Kayombo.

Ameongeza kuwa, watakaotembelea pia wataelekezwa jinsi ya kutoa taarifa kwa wafanyakazi wasio na maadili ili waweze kuchukuliwa hatua.

“Wateja pia tutawaelewesha jinsi ya kuwaripoti wafanyakazi ambao hawana maadili na tunawaelimisha tunachukua hatua gani kwa watu hao ili waweze kufanya kazi kwa maadili,” amesema.

spot_img

Latest articles

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

More like this

Neema Mchau ajitosa kugombea Udiwani Viti Maalum Ilala

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Jukwaa la Wanawake Kata ya Gongolamboto Neema Mchau amechukua fomu...

Amanzi na Babu Tale uso kwa uso Jimboni

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la Chuo...

VETA Pwani yabuni Mita ya Maji ya Kisasa, kutatua migogoro kwa wapangaji

Na Tatu Mohamed KATIKA hatua ya kuleta mageuzi katika usimamizi wa matumizi ya maji...