Lissu ajitetea mwenyewe mahakamani,  awaweka pembeni  mawakili wake 30

Na Mwandishi Wetu

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imekubali maombi ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu la kujitetea mwenyewe katika kesi ya uhaini inayomkabili na kuwaondoa mawakili wake 30 waliokuwa wakimtetea katika kesi hiyo.

Maombi hayo yaliwasilishwa na Lissu mwenyewe mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Franko Kiswaga ambaye alikubali ombi hilo, akieleza kuwa Lissu atakuwa huru kujibu hoja za upande wa mashtaka yeye binafsi hadi pale atakapoamua kuhitimisha utetezi wake.

Lissu ameeleza kuwa hana muda wa kuzungumza na mawakili wake  akiwa gerezani na hataki wabebeshwe lawama kwa lolote litakalotokea.

Amesema kwa siku 68 alizokaa mahabusu imeshindikana kuzungumza na mawakili wake na akaona isiwe sababu ya wao kulaumiwa na kuonekana hawajamtetea ipasavyo.

Ameeleza kuwa  katika siku hizo 68, wiki  moja alikuwa gereza Keko na tangu Ijumaa Kuu alihamishiwa gereza la Ukonga   lakini mawakili wake walikuwa hawaruhusiwi kuzungumza naye kwa faragha wala ruhusa ya kubadilishana nyaraka na wanazungumza kwa simu.

“Kama  mfungwa mwenye mawakili, nina haki ya kuonana na mawakili kwa faragha na si mapenzi ya bwana jela,” amesema Lissu.

Lissu ameiambia Mahakama kuwa amekuwa akipitia mateso na ananyimwa haki ya kuabudu akiwa mahabusu na kusema  kuwa hatua hiyo ni kinyume cha sheria na haki za binadamu na katiba ya nchi wakati wafungwa na mahabusu wengine wakipata haki hiyo.

Hata hivyo Mahakama imeahirisha kesi  hiyo ya uhaini hadi Julai 1, 2025 kwa ajili ya kusubiri Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kupitia jalada la kesi hiyo ili kuona kama iende Mahakama Kuu au hapana.

Hatua hiyo inatokana na upande wa mashtaka kuomba ahirisho mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Kiswaga ambapo Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga alisema jalada la kesi hiyo lipo kwa DPP analipitia kisha atatoa taarifa kuhusu upelelezi ulipofikia na kama kesi hiyo iende Mahakama Kuu au hapana.

Lissu anadaiwa kutenda kosa hilo Aprili 3, 2025 ndani ya Jiji la Dar es Salaam kuwa siku hiyo kwa nia ya uchochezi aliushawishi umma kuzuia kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, huku akitamka na kuandika maneno kumshinikiza kiongozi Mkuu wa Serikali ya Tanzania.

Juni 2, 2025, upande wa mashtaka ulieleza Mahakama kuwa jalada la upelelezi liliwasilishwa kwa DPP lakini baada ya kulipitia alibaini kuwepo kwa mapungufu yaliyohitaji kurekebishwa, hivyo kuwasilisha tena kwa wapelelezi.

Kutokana na hali hiyo, Wakili wa Serikali Nassoro Katuga aliomba mahakama kuahirisha kesi hiyo hadi tarehe nyingine ambapo Hakimu Kiswaga alikubali na kupanga kutajwa tena Julai 1,2025.

spot_img

Latest articles

Rais Samia: MEATU mtaendelea kupata miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo Nishati

📌Asema baada ya Vijiji vyote Meatu kupata umeme kasi inaelekea vitongojini 📌 Ataka umeme utumike...

GFA yaweka rekodi uundaji magari nchini, yakamilisha gari ya 4000

Na Mwandishi Wetu Kiwanda cha kwanza kutengeneza na kuunganisha magari Tanzania cha GF Vehicles Assemblers...

Mwanafunzi wa chuo ashikiliwa Polisi kwa kumuua mwenzake  wakiwa ‘Club’ wamelewa

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha...

Mwanamke ajiua kwa sumu  kisa mapenzi

Na Mwandishi Wetu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi Richard Abwao,  amesema mwanamke mmoja...

More like this

Rais Samia: MEATU mtaendelea kupata miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo Nishati

📌Asema baada ya Vijiji vyote Meatu kupata umeme kasi inaelekea vitongojini 📌 Ataka umeme utumike...

GFA yaweka rekodi uundaji magari nchini, yakamilisha gari ya 4000

Na Mwandishi Wetu Kiwanda cha kwanza kutengeneza na kuunganisha magari Tanzania cha GF Vehicles Assemblers...

Mwanafunzi wa chuo ashikiliwa Polisi kwa kumuua mwenzake  wakiwa ‘Club’ wamelewa

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha...