Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi

BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake la kesho dhidi ya Mnaigeria, Stanley Eribo litakuwa la kisasi, huku Hamad Furahisha akitaka kuweka rekodi ya kumchapa Mmalawi Hanock Phiri.

Mabondia hao wanatarajia kupanda ulingoni kesho Desemba 26, kuzichapa katika pambano lililopewa jina la Boxing On Boxing Day kwenye Ukumbi wa Warehouse, jijjni Dar es Salaam.

Akizungumzia mchezo huo, Mwakinyo amesema kuwa hadi kufikia hatua ya kupima uzito na kila mtu afya yake ipo sawa, hakuna sababu ya kuzuia pambano hilo lisipigwe.

“Kutokana na afya za watu wote hapa ni nzuri, nafikiri hakuna sababu ya kufanya pambano lisipigwe. Mimi sina mengi ya kuongea kisasi kitafanywa,” ametamba Mwakinyo.

Naye Furahisha amesema mpinzani wake anatamba kwa kuwa amewapiga baadhi ya mabondia hapa nchini lakini ajue safari hii atakutana na kitu tofauti na kipigo kinamhusu.

Amesema amesindikizwa na watu wengi kwenda kupima uzito akiwamo diwani, wote wakiwa na imani naye, hivyo hatawaangusha watanzania.

Kwa upande wake Mratibu wa matukio wa Peak Time ambao ni waandaaji wa mapambano yako, Bakari Hatibu, amesema maandalizi yote yamekamilika na mabondia wote waliotakiwa wamefika.

Mapambano mengine Hassan Ndonga atazichapa na Ismail Boyka, Ally Ngwando vs Mussa Makuka
Issa Simba (Kahama) vs Wilson Phiri (Malawi), Debora Mwenda vs Mariam Dick (Malawi) na Leila Machi vs Hidaya Zahoro.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...