Chongolo ‘kuhamia’ Dar

Na Mwandishi Wetu, Media Brains

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo, anatarajia kuhutubia katika mkutano wa hadhara utakaofanyika Dar es Salaam Julai 29,2023 katika viwanja vya Tanganyika Pakers Kawe.

Kufanyika kwa mkutano huo ni utekelezaji wa maazimio ya Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kilichokutana hivi karibuni jijini Dodoma ambacho pamoja na mambo mengine kiliazimia katibu mkuu kufanya mikutano katika mikoa mbalimbali ukiwemo Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari Julai 25,2023 Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Abasi Mtemvu, amesema katika mkutano huo wataeleza utekekezaji wa Ilani ya Uchaguzi uliofanyika Dar es Salaam na maeneo mengine ya nchi.

“Dhamira ya CCM ni kuendelea kuwaletea wananchi maendeleo, tunawaomba wananchi waje kwa wingi kwenye mkutano huu, tutaeleza utekelezaji wa Ilani na mambo mengi yanayoendelea nchini chini ya usimamizi wa Rais Samia Suluhu Hassan,” amesema Mtemvu.

Chongolo anaendelea na ziara yake katika mikoa mbalimbali nchini ambapo tayari amefanya mikutano Mbeya, Mtwara, Lindi, Singida na Arusha.

spot_img

Latest articles

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...

Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani...

More like this

Papa mpya apatikana ni Robert Prevost

Na Mwandishi Wetu Papa Mpya wa Kanisa Katoliki Duniani, ametangazwa ni Kardinali Robert Francis Prevost(69),...

Waziri Masauni, Umoja wa Ulaya wajadili Mazingira

Mwandishi Maalum-Denmark Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhandisi Hamad...

Serikali yasamehe faini za maji, yataka wananchi warejeshewe huduma

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Maji, Jumaa Aweso ametangaza msamaha wa faini zote kwa wananchi...