TFF yamfungia miaka sita Katibu Mkuu DRFA

Na Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA),Ramadhan Missiru amefungiwa na Kamati ya Maadili ya Soka Tanzania (TFF), kutojihusisha na shughuli zozote za mpira wa miguu kwa kipindi cha miaka sita ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa taarifa ya TFF iliyotolewa leo Mei 13, 2025 na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano, Clifford Ndimbo, Missiru alipatikana na hatia ya makosa mawili ya ukiukwaji wa maadili yaliyobainishwa na kamati hiyo katika kikao chake kilichofanyika Mei 8, 2025 jijini Dar es Salaam.

Taarifa hiyo imesema kuwa Missiru alishtakiwa na Sekretarieti ya TFF kwa makosa mawili ikiwemo kushindwa kutii maamuzi ya Kamati ya Maadili, kinyume na Kanuni ya 73(8) ya Maadili ya TFF Toleo la 2021. Kosa lingine ni kuchochea umma, kinyume na Kanuni ya 73(4) ya Maadili ya TFF Toleo la 2021.

“Baada ya Kamati kusikiliza pande zote na kupitia nyaraka na vielelezo vilivyowasilishwa mbele yake. imemtia hatiani kwa makosa mawili na kumpa adhabu ya kumfungia  kijihusisha na masuala ya mpira wa miguu  ndani na nje ya nchi kwa kipindi cha miaka sita na kulipa faini ya sh 5,000,000,”

Kwa upande wa Mkuu wa Idara ya Habari ya na Mawasiliano ya Klabu ya Azam, Thabit Zakaria ‘Zakazakazi’, aliyeshtakiwa katika kamati hiyo kwa kuchochea umma, kamati ilibaini hakuna ushahidi wa kutoasha kumtia hatiani.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...