TFF yamfungia miaka sita Katibu Mkuu DRFA

Na Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA),Ramadhan Missiru amefungiwa na Kamati ya Maadili ya Soka Tanzania (TFF), kutojihusisha na shughuli zozote za mpira wa miguu kwa kipindi cha miaka sita ndani na nje ya nchi.

Kwa mujibu wa taarifa ya TFF iliyotolewa leo Mei 13, 2025 na Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano, Clifford Ndimbo, Missiru alipatikana na hatia ya makosa mawili ya ukiukwaji wa maadili yaliyobainishwa na kamati hiyo katika kikao chake kilichofanyika Mei 8, 2025 jijini Dar es Salaam.

Taarifa hiyo imesema kuwa Missiru alishtakiwa na Sekretarieti ya TFF kwa makosa mawili ikiwemo kushindwa kutii maamuzi ya Kamati ya Maadili, kinyume na Kanuni ya 73(8) ya Maadili ya TFF Toleo la 2021. Kosa lingine ni kuchochea umma, kinyume na Kanuni ya 73(4) ya Maadili ya TFF Toleo la 2021.

“Baada ya Kamati kusikiliza pande zote na kupitia nyaraka na vielelezo vilivyowasilishwa mbele yake. imemtia hatiani kwa makosa mawili na kumpa adhabu ya kumfungia  kijihusisha na masuala ya mpira wa miguu  ndani na nje ya nchi kwa kipindi cha miaka sita na kulipa faini ya sh 5,000,000,”

Kwa upande wa Mkuu wa Idara ya Habari ya na Mawasiliano ya Klabu ya Azam, Thabit Zakaria ‘Zakazakazi’, aliyeshtakiwa katika kamati hiyo kwa kuchochea umma, kamati ilibaini hakuna ushahidi wa kutoasha kumtia hatiani.

spot_img

Latest articles

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

Mkazi wa Magomeni Ashinda Gari Ford Ranger Kupitia Kampeni ya Tembocard ni Shwaa ya CRDB

Na Mwandishi Wetu MKAZI wa Magomeni, Rahabu Mwambene, ameibuka mshindi wa gari aina ya...

Aliyekuwa akiombewa amuua mchungaji wake kwa panga

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara linamshikilia Victor Fransis Thomas (39), mkulima...

Lissu awaambia wafuasi wake wajiandae akitoka ni mchakamchaka

Na Mwandishi Wetu Mwenyekiti wa Chama Cha  Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amewaambia wasuasi na...

More like this

Ofisi ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ya Sabasaba kutangaza huduma

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili Hazina yazitaka taasisi za umma kutumia maonesho ...

Mkazi wa Magomeni Ashinda Gari Ford Ranger Kupitia Kampeni ya Tembocard ni Shwaa ya CRDB

Na Mwandishi Wetu MKAZI wa Magomeni, Rahabu Mwambene, ameibuka mshindi wa gari aina ya...

Aliyekuwa akiombewa amuua mchungaji wake kwa panga

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara linamshikilia Victor Fransis Thomas (39), mkulima...