Waziri Mhagama apiga marufuku maiti kuzuiwa kwa kigezo cha madeni

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Afya, Jenista Mhagama ameziagiza hospitali zote za umma nchini kutekeleza kwa ukamilifu maelekezo yaliyokwishatolewa na Serikali ya kupiga marufuku hospitali na vituo vya afya kuzuia maiti kwa kigezo cha kutolipwa gharama za matibabu.

Waziri Mhagama ametoa agizo hilo mkoani Tabora, wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Chanjo Kitaifa na kuongeza kuwa wahudumu wa afya watakaoendelea kuzuia maiti kuzikwa watachukuliwa hatua za kisheria.

“Kumekuwa na kelele nyingi za upatikanaji wa maiti pale wenzetu wanapotangulia mbele za haki, ninawaomba vituo vyote vinavyotoa huduma za afya nchini maelekezo ya Serikali hayajabadilika, tunao waraka wa mwaka 2021 ambao umetoa maelekezo ya namna gani ya kushughulikia suala zima la huduma kwa maiti pale kifo kinapotokea.

“Ninawaagiza tena Waganga Wafawidhi wote rudini angalieni muongozo tulioutoa acheni kuleta usumbufu kwa wananchi wa Tanzania, hatutaendelea kumfumbia mtu macho ambaye hatozingatia waraka ambao wizara na Serikali uliutoa wa upatikanaji wa maiti pale wenzetu wanapotangulia mbele za haki,” amesema na kuongeza kuwa:

“Wakati mwingine inashangaza, aliyefariki huyo ndiye aliyekuwa na uwezo wa kujihudumia na kujilipia matibabu, waliobaki hawana uwezo, sasa unadai nini huyo marehemu sasa afufuke atoe hela ndio muweze kumuachia?, haiwezekani, naomba fuateni waraka wetu, maelekezo yako wazi, tunashangaa kituo cha afya wapo baadhi ya watu wakifariki mila au imani za dini zinawataka wazikwe haraka tunapochelewesha hiyo michakato tunawakosea haki,”.

spot_img

Latest articles

Mgodi wa kihistoria wa niobium kujengwa Mbeya

Na Mwandishi Mbeya TANZANIA imepiga hatua muhimu katika kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na Marekani baada...

Ndejembi ataka Ewura kukagua maghala ya mafuta kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa

📌Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote 📌Timu...

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

More like this

Mgodi wa kihistoria wa niobium kujengwa Mbeya

Na Mwandishi Mbeya TANZANIA imepiga hatua muhimu katika kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na Marekani baada...

Ndejembi ataka Ewura kukagua maghala ya mafuta kuhakikisha hakuna mafuta yanayofichwa

📌Asema nchi ina usalama mkubwa wa mafuta hivyo wananchi waendelee kupata huduma muda wote 📌Timu...

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...