Mkoa wa Mwanza wawakaribisha wawekezaji, waanika fursa lukuki

Na Winfrida Mtoi, Mwanza

MKOA wa Mwanza umeweka bayana utayari wake wa kutoa maeneo ya uwekezaji kwa watu binafsi na Serikali kutokana na fursa nyingi zinazopatikana katika mkoa huo.

Hayo yameelezwa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Chagu Nghoma alipomwakilisha Mkuu wa Mkoa wa huo, Said Mtanda katika Mdahalo wa Kitaifa uliondaliwa na Kituo cha Ubia wa Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC) wenye Mada Kuu ya ‘Ubia wa Sekta ya umma na Sekta Binafsi katika Muktadha wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 uliofanyika kwenye Ukumbi wa hoteli ya Gold Crest, jijini Mwanza.

Mhandisi Nghoma amesema kuna fursa nyingi ya uwekezaji za kukuza uchumi katika Mkoa huo, ikiwamo sekta ya Uchumi wa Buluu ukilenga ufugaji wa samaki na shughuli nyingine zinazofanyika katika Ziwa Victoria.

Amesema pamoja na hayo pia kuna maeneo mengi yanayofaa kwa ufugaji wa mifungo kama vile Ng’ombe na Mbuzi.

Ameeleza kuwa kuhusu uchumi wa Buluu kuna ufugaji wa samaki ambayo inahitaji kwa kiasi kikubwa uwekezaji wa viwanda na kuwekeza katika chakula cha samaki, pia viwanda vya nyama vinahitajika zaidi.

“Mkoa wa Mwanza una maeneo mengi ya uwekezaji na Mkoa upo tayari kuyatoa maeneo hayo kwa watu binafsi na Serikali. Uchumi wa mtu unaanza na mtu binafsi, ni lazima kufikiria nini unataka kufanya katika kuboresha uchumi binafsi na nchi,” amesema.

spot_img

Latest articles

Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha...

Aishi Manula afunguka ugumu wa kuikabili Uganda

Na Winfrida Mtoi Timu ya Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), imeanza mazoezi kujiandaa...

‎Msigwa: Bwawa la Kidunda ni mradi wa kimkakati kwa Maji, Kilimo na Nishati

Na Mwandishi Wetu Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, ameipongeza Wizara ya Maji kwa...

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

More like this

Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha...

Aishi Manula afunguka ugumu wa kuikabili Uganda

Na Winfrida Mtoi Timu ya Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), imeanza mazoezi kujiandaa...

‎Msigwa: Bwawa la Kidunda ni mradi wa kimkakati kwa Maji, Kilimo na Nishati

Na Mwandishi Wetu Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, ameipongeza Wizara ya Maji kwa...