Kapinga: Vitongoji 9000 kusambaziwa umeme mwaka 2025/26

📌 Majimbo yaendelea kufaidika na mradi wa umeme wa Vitongoji 15

Na Mwandishi Wetu

NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imekamilisha kazi ya kupeleka umeme kwenye Vijiji vyote Tanzania Bara na nguvu sasa inaelekezwa kwenye vitongoji.

Kapinga ameeleza kuwa, pamoja na kazi ya kupeleka umeme vitongojini inayoendelea sasa, Serikali ina mkakati wa kupeleka umeme kwenye Vitongoji 9,000 katika mwaka ujao wa fedha wa 2025/26.

Ameeleza hayo leo Aprili 09, 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la la Mbunge wa Nkansi Kusini, Vicent Mbogo aliyeuliza ni lini Serikali itapeleka umeme katika Vitongoji vilivyopo Jimbo la Nkansi Kusini.

“Kitongoji cha Lupata kilichopo Kata ya Kizumbi kitapata umeme kupitia mradi wa Vitongoji 15 vya kila Mbunge, na kitongoji cha Lwela Kata ya Mpembe kitapata umeme kupitia miradi itakayokuja,” amesema Kapinga.

Akijibu swali Mbunge wa Momba, Condester Sichwale aliyeuliza ni upi mkakati wa Serikali wa kupeleka umeme kwenye Vitongoji vya Tarafa za Ndarambu, Msangano na Kamsambu, Kapinga amesema Serikali inao mkakati wa kutekeleza miradi ya umeme kwenye Vitongoji na hivi sasa inatekeleza mradi wa kupeleka umeme kwenye Vitongoji 15 kwa kila Jimbo.

Ameongeza kuwa katika miradi wa Vitongoji 15 wakandarasi wamemaliza kazi za awali na sasa hivi wapo katika hatua ya kupata vifaa.

spot_img

Latest articles

Ajali ya moto yaua watoto yatima watano

Na Mwandishi Wetu Watoto watano waliokuwa wanalelewa katika kituo cha watoto yatima cha Igambilo Manispaa...

Januari Makamba hayumo, Nape apeta uteuzi CCM

Na Mwandishi wetu Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Rais wa Yanga akatwa uteuzi Jimbo la Kigamboni, Jemedali, Shafii Dauda mambo mazuri

Na Mwandishi Wetu Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Hersi Saidi ameshindwa kupenya katika  uteuzi...

CCM yamtema Luhaga Mpina

Na Mwandishi Wetu MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, hatakuwa miongoni mwa wanaowania ubunge kupitia...

More like this

Ajali ya moto yaua watoto yatima watano

Na Mwandishi Wetu Watoto watano waliokuwa wanalelewa katika kituo cha watoto yatima cha Igambilo Manispaa...

Januari Makamba hayumo, Nape apeta uteuzi CCM

Na Mwandishi wetu Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Rais wa Yanga akatwa uteuzi Jimbo la Kigamboni, Jemedali, Shafii Dauda mambo mazuri

Na Mwandishi Wetu Rais wa klabu ya Yanga, Injinia Hersi Saidi ameshindwa kupenya katika  uteuzi...