Aishi Manula afunguka ugumu wa kuikabili Uganda

Na Winfrida Mtoi

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), imeanza mazoezi kujiandaa na michezo miwili ya Kalenda ya FIFA dhidi ya Uganda na Rwanda, ambapo  kipa wa kikosi hicho Aishi Manula  amesema haitakuwa rahisi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 1, 2026 katika viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam wanapofanyika mazoezi, Manula amesema  timu hizi zina upinzani mkubwa zinapokutana kutokana na ujirani.

Amebainisha kuwa  michezo inayokutanisha timu za ukanda mmoja huwa  hazitabiriki kwa sababu hakuna timu inayokubali unyonge mbele ya jirani yake, hali inayoongeza presha na uzito wa michezo hiyo.

​”Nadhani ujirani tulionao ndio utakaosababisha mechi ziwe ngumu zaidi kwa sababu kila mmoja anahitaji kupata ushindi ili kuendelea kujiona yuko kwenye nafasi bora zaidi ya mwenzake,”  amesema.

​Taifa Stars itavaana na Uganda  Juni 5, kisha Rwanda Juni 9, 2026

spot_img

Latest articles

Zawadi ya gari yawapa mzuka mabondia

Na Winfrida Mtoi Waandaaji wa pambano la Dar Boxing Derby wameweka gari aina ya Crown...

Nani anajali kurejesha hadhi Tanzania?

WIKI iliyopita haikuwa ya habari njema kwa Taifa la Tanzania huko duniani. Pamoja na...

TCAA YAIMARISHA HUDUMA KWA WATEJA KUPITIA DAWATI MAALUM

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kupitia kwa Mkurugenzi wake...

TBA YASHINDA TUZO YA BANDA BORA SABASABA, YATANGAZA DIRA YA KUFIKIA VIWANGO VYA KIMATAIFA

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umeibuka mshindi wa pili na kutunukiwa tuzo...

More like this

Zawadi ya gari yawapa mzuka mabondia

Na Winfrida Mtoi Waandaaji wa pambano la Dar Boxing Derby wameweka gari aina ya Crown...

Nani anajali kurejesha hadhi Tanzania?

WIKI iliyopita haikuwa ya habari njema kwa Taifa la Tanzania huko duniani. Pamoja na...

TCAA YAIMARISHA HUDUMA KWA WATEJA KUPITIA DAWATI MAALUM

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kupitia kwa Mkurugenzi wake...