Majaliwa azindua Kituo cha Mabasi Nzega Mjini

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Machi 13, 2025 amezindua kituo kipya cha Mabasi cha Nzega mjini ambacho ujenzi wake umegharimu shilingi bilioni 4.327.

Akizungumza baada ya kuzindua kituo hicho ambacho utekelezaji wake umefikia asilimia 100, Majaliwa ameipongeza Halmashauri hiyo kwa uamuzi wa ujenzi wa kituo hicho kwani kitaibua fursa za biashara kwa wakazi wa eneo hilo.

“Kituo hiki ni kizuri na kimejengwa kwa ubora, kituo hiki kinatakiwa kianze kutumika ili wananchi waanze kunufaika nacho, Watumishi wa halmashauri ongozeni Wana-Nzega kunufaika na fursa katika eneo lenu,” amesema.

Aidha, Majaliwa ametoa wito kwa Halmashauri hiyo kuongeza vibanda vya wafanyabiashara badala ya vichache ambavyo vimejengwa mpaka sasa.

“Tunataka wananchi wengi zaidi wanufaike, ongezeni vibanda, huu ni ubunifu mzuri sana utasababisha wengi wanufaike, waleteni wajasiriamali hapa wapate rizki zao, mkifanya hivyo mtaongeza mzunguko wa fedha,” amesema

Majaliwa amefafanua kuwa Serikali inaendelea na mpango kazi wake wa kuwahudumia watanzania wakati wote.

Katika hatua nyingine, Majaliwa ametoa wito kwa watumishi wa halmashauri nchini kuendelea kujielekeza katika kutatua changamoto za wananchi.

spot_img

Latest articles

Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha...

Aishi Manula afunguka ugumu wa kuikabili Uganda

Na Winfrida Mtoi Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), imeanza mazoezi kujiandaa na michezo...

‎Msigwa: Bwawa la Kidunda ni mradi wa kimkakati kwa Maji, Kilimo na Nishati

Na Mwandishi Wetu Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, ameipongeza Wizara ya Maji kwa...

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

More like this

Kibabage aimpa mzuka Serengeti Boys kuelekea fainali ya AFCON

Na Winfrida Mtoi BEKI wa timu ya Taifa (Taifa Stars), Nickson Kibabage amesema kitendo cha...

Aishi Manula afunguka ugumu wa kuikabili Uganda

Na Winfrida Mtoi Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), imeanza mazoezi kujiandaa na michezo...

‎Msigwa: Bwawa la Kidunda ni mradi wa kimkakati kwa Maji, Kilimo na Nishati

Na Mwandishi Wetu Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, ameipongeza Wizara ya Maji kwa...