Majaliwa azindua Kituo cha Mabasi Nzega Mjini

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Machi 13, 2025 amezindua kituo kipya cha Mabasi cha Nzega mjini ambacho ujenzi wake umegharimu shilingi bilioni 4.327.

Akizungumza baada ya kuzindua kituo hicho ambacho utekelezaji wake umefikia asilimia 100, Majaliwa ameipongeza Halmashauri hiyo kwa uamuzi wa ujenzi wa kituo hicho kwani kitaibua fursa za biashara kwa wakazi wa eneo hilo.

“Kituo hiki ni kizuri na kimejengwa kwa ubora, kituo hiki kinatakiwa kianze kutumika ili wananchi waanze kunufaika nacho, Watumishi wa halmashauri ongozeni Wana-Nzega kunufaika na fursa katika eneo lenu,” amesema.

Aidha, Majaliwa ametoa wito kwa Halmashauri hiyo kuongeza vibanda vya wafanyabiashara badala ya vichache ambavyo vimejengwa mpaka sasa.

“Tunataka wananchi wengi zaidi wanufaike, ongezeni vibanda, huu ni ubunifu mzuri sana utasababisha wengi wanufaike, waleteni wajasiriamali hapa wapate rizki zao, mkifanya hivyo mtaongeza mzunguko wa fedha,” amesema

Majaliwa amefafanua kuwa Serikali inaendelea na mpango kazi wake wa kuwahudumia watanzania wakati wote.

Katika hatua nyingine, Majaliwa ametoa wito kwa watumishi wa halmashauri nchini kuendelea kujielekeza katika kutatua changamoto za wananchi.

spot_img

Latest articles

Sakata lake na Harmonize, Ibraah aiachia Basata

Na Mwandishi Wetu Baada ya kutoka ofisi za Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), msanii...

Waziri Mkuu ashiriki ufunguzi wa jukwaa la maafisa watendaji wakuu Afrika 2025

Na Mwandishi Wetu WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameshiriki ufunguzi wa Mkutano wa siku mbili...

TFF kuja mshirika wa kubashiri mechi zake

Na Mwandishi Wetu Shirikisho wa Soka Tanzania(TFF),limesema kuanzia msimu ujao wa 2025/2026 litakuwa na mshirika...

Viongozi mbalimbali washiriki ibada ya kuaga mwili wa Cleopa Msuya

Viongozi mbalimbali wa Serikali na wananchi wakiaga mwili wa aliyekuwa Makamu wa kwanza wa...

More like this

Sakata lake na Harmonize, Ibraah aiachia Basata

Na Mwandishi Wetu Baada ya kutoka ofisi za Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), msanii...

Waziri Mkuu ashiriki ufunguzi wa jukwaa la maafisa watendaji wakuu Afrika 2025

Na Mwandishi Wetu WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameshiriki ufunguzi wa Mkutano wa siku mbili...

TFF kuja mshirika wa kubashiri mechi zake

Na Mwandishi Wetu Shirikisho wa Soka Tanzania(TFF),limesema kuanzia msimu ujao wa 2025/2026 litakuwa na mshirika...