Watumishi Tume ya Madini wajengewa uwezo matumizi ya mashine za kupima madini ya metali

Na Mwandishi Wetu

KATIBU Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Ramadhani Lwamo amewataka watumishi wa Tume kufanya kazi kwa kujituma na weledi hasa kwenye usimamizi wa shughuli za uchimbaji, uchenjuaji na biashara ya madini ili Sekta ya Madini iendelee kuwa na mchango mkubwa kwenye Pato la Taifa.

Mhandisi Lwamo ametoa rai hiyo, leo Februari 25, 2025 jijini Dodoma akifungua mafunzo ya matumizi ya mashine maalum za kupima madini ya metali kwa njia ya Mionzi /X-RAY kwa watalam wa Tume ya Madini wakiwemo Wahandisi Migodi, Wahasibu, Watakwimu, Maafisa Utawala na Wataalam wa Maabara ‘Lab Technologist.

Amesema kuwa, tangu kuanzishwa kwa Tume ya Madini rekodi ya makusanyo ya maduhuli ya Serikali imeendelea kukua hali iliyopelekea wadau wengi wa madini na wananchi kwa ujumla kuwa na taswira chanya ya Tume.

“Mwaka wa fedha uliopita 2023/2024 tulimaliza kwa kukusanya Shilingi Bilioni 753, mwaka huu tunatakiwa kukusanya Shilingi Trilioni Moja, sote tunapaswa kuwa na weledi ili tuweze kufikia lengo, hatuwezi kufika bila uadilifu, kujituma na kutunza vitendea kazi,” amesema Mhandisi Lwamo.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Lwamo amesema kuwa Serikali kupitia Tume ya Madini itaendelea kuboresha mazingira ya utendaji kazi kwa Ofisi za Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa, Masoko ya Madini, Vituo vya Ununuzi wa Madini na Maabara ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa vitendea kazi vya kutosha na kutatua changamoto zinazowakabili wachimbaji wa madini nchini.

Naye Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini, Venance Kasiki amesema lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha watumishi wanajengewa uwezo wa matumizi sahihi ya mashine za kupima madini ya metali ambazo kwa kiasi kikubwa zimesaidia sana kudhibiti upotevu wa mapato ya Serikali.

spot_img

Latest articles

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...

Rais Samia: Walilenga kupindua dola

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema kuwa vurugu...

More like this

Waziri wa Nishati Ndejembi azindua rasmi mita janja

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi amezindua rasmi mita janja (smart meter)...

RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima...

Tume ya Jaji Chande na mlima wenye utelezi

KAMA kuna tume ya uchunguzi iliyopata kuundwa nchini kwa jambo mahususi, ikajikuta katika uwanja...