Majaliwa aeleza msimamo wa Tanzania baada ya kauli ya Trump kusitisha misaada

Na Mwandishi Wetu

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ameeleza msimamo wa Serikali ya Tanzania kuhusu mabadiliko ya sera za misaada ya Marekani chini ya utawala wa Rais Donald Trump, akisisitiza kuwa Tanzania lazima ijikite katika kujitegemea kiuchumi.

Akizungumza bungeni jijini Dodoma leo, Alhamisi Februari 6, 2025, Majaliwa amesema kuwa Marekani, kupitia Shirika lake la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), imesitisha baadhi ya misaada iliyokuwa ikitolewa kwa Tanzania na nchi nyingine zinazoendelea.

Amesema kuwa mabadiliko hayo ni sehemu ya sera mpya za mambo ya nje za Marekani, ambazo zinaweza kuwa na athari kwa baadhi ya sekta nchini.

“Ni kweli kwamba Serikali yetu inaheshimu sera za mambo ya nje na tunatekeleza mikataba kwa mujibu wa makubaliano na nchi husika. Hata hivyo, tumeanza kuona mabadiliko katika sera za baadhi ya nchi zenye uwezo mkubwa kama Marekani na haya mabadiliko yanaweza kuathiri baadhi ya nchi ikiwemo Tanzania,” amesema Majaliwa.

Pamoja na hilo, Majaliwa amesisitiza kuwa Tanzania imejipanga kuhakikisha kuwa uchumi wake unajitegemea ili kuepuka utegemezi wa misaada ya nje.

spot_img

Latest articles

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...

Mwigizaji, msanii wa Bongo Flava wafariki dunia

Na Mwandishi Wetu MSANII wa filamu nchini, Hashim Kambi, amefariki dunia leo alasiri akiwa anapatiwa...

More like this

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...