Doyo kugombea uenyekiti ADC, amkaribisha Mchungaji Msigwa

Na Winfrida Mtoi

Katibu Mkuu wa Chama cha  Alliance for Democratic Change (ADC), Doyo Hassan Doyo ametangaza dhamira ya kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama hicho Taifa baada ya Hamad Rashid Mohammed kumaliza muda wake.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 6, 2024 jijini Dar es Salaam, Doyo amesema anatangaza kugombea nafasi hiyo kwa kuamini  ana uwezo wa kukitumikia chama hicho katika kutekeleza matakwa ya Katiba.

“Mimi nimejipanga kuwa mwenyekiti wa chama hiki ili kurithi mikoba ya Mheshimiwa  Hamadi Rashid kwa sababu  nimepata mafunzo makubwa sana kutoka kwake. Huyu ni mwanasiasa mzoefu na amefanya kazi na wanasiasa wakongwe,” amesema Doyo.

Amesema Hamad amewafunza jambo katika chama hicho kwani ameonyesha kufuata matakwa ya Katiba kwa  kuachia ngazi baada ya kumaliza muda wake na kuwapa funzo vijana wa chama hicho na wana siasa wengine nchini.

Doyo ameeleza kuwa kati ya mafunzo aliyopata kutoka kwa mwanasiasa huyo mkongwe ni uvumilivu na kupambana na kila changamoto.

Katika hatua nyingine, amemkaribisha Mchungaji Peter  Msigwa wa  Chadema kujiunga na chama hicho endapo haridhishwi na mambo yanavyokwenda huko aliko.

spot_img

Latest articles

Hatuna pa kujificha, tuwajibike tu yaishe

TAIFA la Tanzania ni nchi huru iliyojitawala kwa takribani miaka 65 sasa, tangu bendera...

MD TWANGE ATOA RAI KWA MAMENEJA TANESCO KUONGEZA KASI YA KUPAMBANA NA WIZI WA MIUNDOMBINU YA UMEME

📌Afungua Mkutano Mkuu wa mwaka wa Mameneja na Wakurugenzi wa Kanda, Dodoma 📌Asisitiza umuhimu wa...

Yanga yakomaa kileleni, Simba yavizia ikitafuna  miwa Morogoro

Na Mwandishi Wetu WANANCHI Yanga wamejiweka kwenye nafasi nzuri ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu...

WIZARA YA NISHATI YAENDELEA KUTUMIA NISHATI SAFI EXPO KUTOA ELIMU KWA WANANCHI

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Nishati inaendelea kutoa elimu ya nishati safi ya kupikia...

More like this

Hatuna pa kujificha, tuwajibike tu yaishe

TAIFA la Tanzania ni nchi huru iliyojitawala kwa takribani miaka 65 sasa, tangu bendera...

MD TWANGE ATOA RAI KWA MAMENEJA TANESCO KUONGEZA KASI YA KUPAMBANA NA WIZI WA MIUNDOMBINU YA UMEME

📌Afungua Mkutano Mkuu wa mwaka wa Mameneja na Wakurugenzi wa Kanda, Dodoma 📌Asisitiza umuhimu wa...

Yanga yakomaa kileleni, Simba yavizia ikitafuna  miwa Morogoro

Na Mwandishi Wetu WANANCHI Yanga wamejiweka kwenye nafasi nzuri ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu...