Doyo kugombea uenyekiti ADC, amkaribisha Mchungaji Msigwa

Na Winfrida Mtoi

Katibu Mkuu wa Chama cha  Alliance for Democratic Change (ADC), Doyo Hassan Doyo ametangaza dhamira ya kugombea nafasi ya uenyekiti wa chama hicho Taifa baada ya Hamad Rashid Mohammed kumaliza muda wake.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 6, 2024 jijini Dar es Salaam, Doyo amesema anatangaza kugombea nafasi hiyo kwa kuamini  ana uwezo wa kukitumikia chama hicho katika kutekeleza matakwa ya Katiba.

“Mimi nimejipanga kuwa mwenyekiti wa chama hiki ili kurithi mikoba ya Mheshimiwa  Hamadi Rashid kwa sababu  nimepata mafunzo makubwa sana kutoka kwake. Huyu ni mwanasiasa mzoefu na amefanya kazi na wanasiasa wakongwe,” amesema Doyo.

Amesema Hamad amewafunza jambo katika chama hicho kwani ameonyesha kufuata matakwa ya Katiba kwa  kuachia ngazi baada ya kumaliza muda wake na kuwapa funzo vijana wa chama hicho na wana siasa wengine nchini.

Doyo ameeleza kuwa kati ya mafunzo aliyopata kutoka kwa mwanasiasa huyo mkongwe ni uvumilivu na kupambana na kila changamoto.

Katika hatua nyingine, amemkaribisha Mchungaji Peter  Msigwa wa  Chadema kujiunga na chama hicho endapo haridhishwi na mambo yanavyokwenda huko aliko.

spot_img

Latest articles

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

More like this

Tanesco yagusa mioyo ya watoto wenye mahitaji maalum

📌Ni sehemu ya uwajibikaji wake kwa jamii 📌Yatoa misaada mbalimbali kwa vituo vitatu Dar...

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...