Timu ya Taifa kriketi ya wanawake kusaka tiketi ya kucheza Kombe la Dunia

Na Mwandishi Wetu

Timu ya Taifa ya wanawake ya mchezo wa kriketi ya Tanzania inatarajiwa kushiriki mashindano ya kufuzu Kombe la Dunia yatakayofanyika nchini Namibia kuanzia Agosti 30 hadi 5 Septemba 2025.

Mashindano hayo yanatarajiwa kushirikisha nchi nane kutoka Kanda ya Afrika ambazo ni Nigeria, Namibia, Kenya, Rwanda, Tanzania, Botswana na Uganda, ambazo zitachuana kuwania nafasi ya hatua za juu.

Kwa mujibu wa Shirikisho la Kriketi Tanzania (TCA), kikosi cha Tanzania kimejiandaa vyema na kipo tayari kwa ushindani mkubwa ili kuhakikisha kinapata nafasi ya kuiwakilisha nchi katika hatua zinazofuata za michuano ya dunia.

Wachezaji wa kikosi hicho wametoa wito kwa watanzania kuwapa sapoti ya hali na mali, wakibainisha kuwa uwepo wa mashabiki na hamasa kutoka nyumbani utawapa nguvu zaidi ya kupambana uwanjani.

Mashindano hayo yanachukuliwa kuwa hatua muhimu katika kuendeleza mchezo wa kriketi barani Afrika na kutoa nafasi kwa wachezaji chipukizi kuonyesha vipaji vyao, huku Tanzania ikitarajia kutumia mashindano haya kuinua hadhi ya mchezo huo nchini.

spot_img

Latest articles

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...

DCEA yakamata Tani 9.93 za Dawa za Kulevya, Watuhumiwa 151 Watiwa Mbaroni

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani...

More like this

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...