Ratiba ya Ligi Kuu msimu wa 2025/26 hadharani, Dabi ya Kariakoo Des 13

Na Winfrida Mtoi

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara(TPLB) leo  Agosti 29, 2025,  imetangaza ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ya 2025/26, ikitarajia kuanza rasmi Septemba 17, 2025 na kutamatika Mei 23, 2026,  huku mchezo wa Dabi ya Karikoo Yanga dhidi ya Simba utapigwa Desemba  13, 2025, Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Mchezo wa raundi ya pili wa watani hao wa jadi ambao mwenyeji atakuwa Simba, utapigwa Aprili 04,2026 kwenye dimba uwanja huo.

Mechi za ufunguzi za msimu huu mpya, KMC itaikaribisha Dodoma Jiji Uwanja wa KMC Complex, Mwenge wakati Coastal Union itakuwa mwenyeji wa Tanzania Prisons katika dimba la Mkwakwani, Tanga.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa TPLB, Ibrahim Mwayela amesema ratiba hiyo imezingatia kalenda ya mashindano yote ya ndani na Kimataifa ili kuhakikisha ligi hiyo inakwenda vizuri na kumalizika Mei 23, 2026 kama ilivyopangwa.

 “Ligi yetu inakwenda kuanza rasmi. Tunaamini utakuwa ni msimu mzuri wenye ushindani mkubwa kwa sababu timu zote zimejiandaa na zimesajili vizuri sana na maandalizi yanaendelea,” amesema.

Ratiba yote ya Ligi Kuu Tanzania Bara hii hapa https://www.ligikuu.co.tz

spot_img

Latest articles

Okello awapa jeuri mashabiki wa Yanga

Na Mwandishi Wetu Nyota wa Yanga, Allan Okello amewahakikishia mashabiki wa timu hiyo kuwa watamaliza...

Minziro akabidhiwa Fountain Gate FC

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Fountain Gate FC imemtangaza Fred Felix Minziro kuwa Kocha Mkuu...

Makonda asimamisha uongozi TOC, Rage akabidhiwa jukumu

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesimamisha uchaguzi wa...

Nani amwambie Rais Samia: ‘Name and Shame’ bila vyombo vya habari imara haifui dafu

SUALA la utawala bora halijawahi kuwa eneo rahisi katika uendeshaji na usimamizi wa ofisi...

More like this

Okello awapa jeuri mashabiki wa Yanga

Na Mwandishi Wetu Nyota wa Yanga, Allan Okello amewahakikishia mashabiki wa timu hiyo kuwa watamaliza...

Minziro akabidhiwa Fountain Gate FC

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Fountain Gate FC imemtangaza Fred Felix Minziro kuwa Kocha Mkuu...

Makonda asimamisha uongozi TOC, Rage akabidhiwa jukumu

Na Mwandishi Wetu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesimamisha uchaguzi wa...