Mufti Zubeir asisitiza upendo, kupuuza wanaoneza chuki za kidini mtandaoni

Na Mwandishi Wetu

MUFTI na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir Bin Ally ametoa rai dhidi ya vitendo vya kueneza chuki za kidini kupitia mitandao ya kijamii, akiwataka waumini wa dini ya Kiislamu na Watanzania kwa ujumla kupuuza watu wanaochochea migogoro ya kidini.


Ametoa rai hiyo wakati akitoa tamko la maazimio ya kikao cha Baraza la Ulamaa kilichoketi Machi 4, 2026 katika Makao Makuu ya BAKWATA, Dar es Salaam.

Amesema baadhi ya watu wamekuwa wakitumia mitandao ya kijamii kuchapisha ujumbe wa kumtukana Mtume Muhammad (S.A.W), kuukashifu Uislamu na kuibeza dini hiyo, huku akisisitiza kuwa Waislamu wasichokozeke na watu hao.

“Tunaamini wanaofanya hayo si Wakristo wala watu wa dini nyingine, bali ni watu wenye nia ovu ya kutuchonganisha ili tugombane na kutia mtafaruku kati yetu na dini nyingine na jamii kwa ujumla. Niwasihi Waislamu wasiingie kujibizana kwa sababu watu hao wanataka kueneza chuki na fitna dhidi ya dini nyingine,” amesema Sheikh Mkuu.

Aidha, Mufti wa Tanzania amewataka Waislamu wote nchini wakiwemo Masheikh, wanazuoni, maustadh, maimamu na waalimu wa dini kuendelea kuishi kwa upendo, kuvumiliana na kulinda umoja wa kitaifa uliodumu kwa muda mrefu.

Amesisitiza kuwa mafundisho ya Mtume Muhammad (S.A.W) yanahimiza kuishi kwa wema na watu wa dini nyingine.

Katika hatua nyingine Mufti Zubeir amewataka waislamu na watanzania kwa ujumla kuendelea kuchukua tahadhari kufuatia maelekezo ya serikali juu ya magonjwa ya Uviko-19, homa ya ini, dengue na kipindupindu, akiwatakia muendeleo wa mfungo mwema waumini wote wa dini ya Kiislamu wanaoendelea na mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.

spot_img

Latest articles

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...

Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa...

Vunjabei, Sara kuisaka heshima ya Tanzania One ulingoni

Na Winfrida Mtoi MABONDIA wa ngumi za kulipwa, Halima Ramadhani maarufu Vunjabei na Sara Alex...

More like this

UWT Makangarawe watoa msaada kwa watoto wenye mahitaji maalum kuelekea Siku ya Wanawake Duniani

Na Tatu Mohamed KATIKA kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Umoja wa Wanawake...

‘Makomandoo’ wazitia hasara Simba na Yanga

Na Mwandishi Wetu KLABU za Simba na Yanga zimetozwa faini ta sh.5,000,000 kila moja kwa...

Mwamuzi aliyekataa bao la Simba Zanzibar afungiwa

Na Mwandishi Wetu MWAMUZI Kassim Mpanga Mpanga wa Dar es Salaam, amefungiwa miezi sita  kosa...