RC Kunenge: Mto Ruvu ubaki kwa matumizi ya binadamu tu, tusitishe shughuli nyingine kwa muda

Na Mwandishi Wetu

MKUU wa Mkoa wa Pwani, Abubakar Kunenge, ametoa wito kwa wakulima wanaotumia maji ya Mto Ruvu kwa shughuli za kilimo kusitisha matumizi hayo kwa muda hadi pale mvua zitakapoanza kunyesha kwa wingi ili kutoathiri shughuli za uzalishaji na usambazaji wa maji kwa wananchi wa Dar Es Salaam na Pwani.

Kunenge ametoa wito huo wakati alipofanya ziara katika mitambo ya uzalishaji maji ya Ruvu Chini na Ruvu Juu kwa lengo la kukagua Hali ya uzalishaji maji na upatikanaji wa maji katika chanzo cha mto Ruvu.

“Mabadiliko ya hali ya hewa hususani kuongezeka kwa joto yamesababisha kupungua kwa kiwango cha maji, hususan katika eneo la Ruvu Chini, halii hii pia imesababishwa na shughuli za kilimo zisizo rasmi kando kando ya mto kwa watu kulima bila vibali” ameeleza Kunenge.

Kunenge ameongeza kuwa ,uzalishaji wa maji katika mtambo wa Ruvu Chini umepungua, japokuwa si kwa kiwango kikubwa, huku Ruvu Juu ikiendelea kuwa na kiwango cha maji cha kuridhisha.

“Nitoe wito kwa watumiaji wa maji, hususani wanaofanya Kilimo kusitisha matumizi hayo kwa muda mpaka pale mvua zitakapoanza Tena na maji kuongezeka mtoni, kwasasa maji haya yabaki Kwa matumizi ya binadamu tu, lakini pia tutafatilia wale wanaofanya kilimo kwa kutumia maji ya mto huu bila vibali na kusababisha changamoto katika mto” amesema Kunenge.

Vile vile Kunenge amesema, kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa Bwawa la Kidunda kutasaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa changamoto ya upungufu wa maji, kwani bwawa hilo litaruhusu uhifadhi wa maji ya kutosha bila kutegemea mvua za msimu.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya maji Mhandisi Mwajuma Waziri amewataka Bonde la maji Wami-Ruvu kwa kushirikiana na DAWASA kufanya jitihada za haraka na upesi kuboresha maeneo yenye changamoto katika mto Ruvu yanayopelekea maji kupotea na kupunguza wingi wa maji mtoni ili wananchi wananchi waendelee kupata huduma ya maji yenye uhakika.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...