Chuo cha Malya chawafunda wakufunzi wa gym

Na Winfrida Mtoi

CHUO cha Maendeleo ya Michezo Malya kinaendesha mafunzo maalum kwa wakufunzi wa gym  na makocha wa viungo ili kuwaongezea ujuzi na  kufahamu mbinu mbalimbali zitakazowasaidia kufanya kazi yao kwa weledi.

Mafunzo hayo yaliyoanza Novemba 24,2025 yanayoendelea katika ukumbi wa Uwanja wa Mkapa, jijini Dar es Salaam, yanahusisha washiriki 30 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania.

Akizungumzia lengo la kutoa mafunzo hayo, Makamu wa Mwenyekiti wa Chuo hicho, Salumu Mtumbuka amesema ni kutokana na kukua kwa michezo na  maeneo ya gym ndiyo watu wengi wanapenda kwenda kufanya mazoezi.

“Tumeona tutoe mafunzo haya kwa makocha  wa viungo wa michezo yote na wataalamu wa  gmy ambao wanafundisha watu kufanya mazoezi,  hii itasaidia kutoa elimu yao kitaalamu zaidi.

“Tutaendelea kutoa mafunzo ya michezo kwa lengo ya kupata wataalum ambao wataleta maendeleo katika Taifa letu, pia nina imani elimu hii ambayo washiriki wanapatiwa itaongeza nguvu katika mazoezi yao, “ameeleza.

Kwa upande wake mshiriki wa mafunzo hayo, Peter Pingo amesema elimu aliyoipata itamuongezea ubora katika kazi yake ya kufundisha mazoezi gym.

“Naishukuru Serikali chini ya Chuo ya Malya ambao wametoa kozi hii ambayo itatuongezea weledi na ufanisi wa kazi yetu, nina imani nitakuwa bora zaidi katika kuhakikisha watu wanapata mazoezi yenye viwango vizuri, ” ameeleza.

spot_img

Latest articles

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

More like this

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...