Bondia Mrembo apewa Mmalawi

Na Mwandishi Wetu

BONDIA Debora Mwenda maarufu Bondia Mrembo, ameahidi kuiwakilisha vizuri Tanzania dhidi ya Mariam Dick kutoka Malawi watakapokutana katika pambano la Box on Boxing Day Desemba 26,2025, Warehouse Masaki Dar es Salaam.

Akizungumza leo Novemba 26, 2025, Debora amesema itakuwa  mara yake ya kwanza  kucheza pambano la kimataifa lakini anawaahidi watanzamia kuonesha mchezo mzuri na kuibuka na ushindi wa kishindo.

“Nashukuru kwa nafasi hii niliyoipata, ya kuonesha kitu nilichonacho, nimejiandaa vyakutosha nataka kuwaonesha watanzania kuwa najua kuufanya mchezo huu hata zaidi ya mwanaume,”

Amesema hana woga wowote kwa sababu amewekeza nguvu zake zaidi katika mazoezi na kila siku zinavyokwenda anazidi kuwa bora.

‎Naye mwalimu wa bondia huyo, Dickson Tembo amesema, anaendelea na mazoezi ya kibabe,hivyo watanzania wajiandae kushangilia ushindi wa kishindo siku hiyo.

spot_img

Latest articles

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...

Chipukizi wa kuogelea kushindana ‘ East Africa Development Swimming Gala’

Na Mwandishi Wetu ZAIDI ya waogeleji 600 wanatarajiwa kushiriki katika mashindano ya kuogelea ya chipukizi...

More like this

Muswada wa Sheria ya Uwekezaji wa Umma kukamilika 2026/27

Na Mwandishi wetu KATIKA kuendelea kuimarisha uwekezaji wa umma, Serikali imepanga kukamilisha Muswada wa...

Kocha Bilo afariki dunia

Na Mwandishi Wetu MMILIKI wa Kituo cha Soka cha Bilo Jijini Mwanza, Kocha Athuman Bilal...

Tukatae kunyweshwa sumu hii

“Kama taifa letu lilipata kuwa na bahati ni kuwa na Rais aliyechukia rushwa kama...