Simba yaachia pointi tatu kwa Mkapa, Azam nayo mambo magumu

Na Winfrida Mtoi

Simba imeshindwa kutamba nyumbani baada ya kufungwa na Petro de Luanda bao 1-0 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijjni Dar es Salaam.

Matokeo hayo yamewafanya mashabiki wa timu hiyo waliojitokeza kwa wingi kuondoka kwa unyonge uwanjani wakiwa hawaamini kilichotokea.

Wikiendi ijayo Simba itakuwa ugenini nchini Mali kuikabili Stade Malien ambayo jana ilitoka suluhu na Esperance ya Tunisia.


Wawakilishi wengine wa Tanzania katika Kombe la Shirikisho Afrika, Azam FC wameanza vibaya hatua ya makundi ya michuano hiyo kwa kufungwa ugenini mabao 2-0 na AS Maniema ya DR Congo.

Kati ya wawakilishi wanne wa Tanzania katika michuano hiyo ya CAF yaani Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la. Shirikisho, Yanga pekee ndio imeanza vizuri kwa ushindi wa bao 1-0 dhidi ya FAR Rabat ya Morocco, wakati Singida Bs ikipoteza ugenini kwa kufungwa 2-0 na CR Belouizdad

spot_img

Latest articles

“MADEREVA TANESCO KUWENI CHACHU UTOAJI HUDUMA BORA”

📌Watakiwa kutunza vyombo vya usafiri ili kuongeza ufanisi wa huduma 📌TANESCO yanunua vyombo vya usafiri...

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

More like this

“MADEREVA TANESCO KUWENI CHACHU UTOAJI HUDUMA BORA”

📌Watakiwa kutunza vyombo vya usafiri ili kuongeza ufanisi wa huduma 📌TANESCO yanunua vyombo vya usafiri...

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...