Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi

BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama tatu muhimu katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi AS FAR Rabat.

Ushindi huo wa bao 1-0, walioupata Wanajangwani hao kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar unaifanya timu kuingia katika mchezo wa pili na matumaini ya kuendelea kufanya vizuri.

Yanga inayonolewa na kocha raia wa Ureno, Pedro Goncalves, itacheza mechi ya pili ya michuano hiyo ugenini Ijumaa ijayo dhidi ya JS Kabylie ya nchini Algeria.

Katika hatua nyingine mshambuliaji wa Yanga, Clement Mzize amepokea tuzo yake ya bao bora Afrika mwaka 2025 iliyotolewa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Novemba 19,2025 nchini Morocco.

Mzize alishindwa kwenda Morocco kuhudhuria halfa ya utoaji tuzo hizo kutokana na hali yake ya kiafya.

spot_img

Latest articles

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...

TIRDO yasajili Viwanda 25,650, Yaongeza Maabara za Kisasa Kuimarisha Sekta ya Viwanda

Na Mwandishi Wetu WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia Shirika la Utafiti na Maendeleo ya...

More like this

DCEA yateketeza kilo 504.36 za Heroin Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtwara MAMLAKa ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imeteketeza...

Mkurugenzi wa Rasilimali Watu Tanesco awahakikishia ushirikiano maafisa huduma kwa wateja

📌 Afunga Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Maafisa hao 📌 Awapongeza kwa utendaji bora wenye...

Makonda  awajibu wanaoponda ziara ya Rio

Na Winfrida Mtoi WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema ziara ya...