Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi

BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama tatu muhimu katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi AS FAR Rabat.

Ushindi huo wa bao 1-0, walioupata Wanajangwani hao kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar unaifanya timu kuingia katika mchezo wa pili na matumaini ya kuendelea kufanya vizuri.

Yanga inayonolewa na kocha raia wa Ureno, Pedro Goncalves, itacheza mechi ya pili ya michuano hiyo ugenini Ijumaa ijayo dhidi ya JS Kabylie ya nchini Algeria.

Katika hatua nyingine mshambuliaji wa Yanga, Clement Mzize amepokea tuzo yake ya bao bora Afrika mwaka 2025 iliyotolewa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Novemba 19,2025 nchini Morocco.

Mzize alishindwa kwenda Morocco kuhudhuria halfa ya utoaji tuzo hizo kutokana na hali yake ya kiafya.

spot_img

Latest articles

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

Msajili wa Hazina, Fitch Ratings watathmini mageuzi ya taasisi za umma

Na Mwandishi wa OTR OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) Jumanne, Agosti 11, 2026, ilifanya...

More like this

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...