Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi

BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama tatu muhimu katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi AS FAR Rabat.

Ushindi huo wa bao 1-0, walioupata Wanajangwani hao kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar unaifanya timu kuingia katika mchezo wa pili na matumaini ya kuendelea kufanya vizuri.

Yanga inayonolewa na kocha raia wa Ureno, Pedro Goncalves, itacheza mechi ya pili ya michuano hiyo ugenini Ijumaa ijayo dhidi ya JS Kabylie ya nchini Algeria.

Katika hatua nyingine mshambuliaji wa Yanga, Clement Mzize amepokea tuzo yake ya bao bora Afrika mwaka 2025 iliyotolewa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Novemba 19,2025 nchini Morocco.

Mzize alishindwa kwenda Morocco kuhudhuria halfa ya utoaji tuzo hizo kutokana na hali yake ya kiafya.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...