Dube awapa raha wananchi

Na Winfrida Mtoi

BAO pekee lililofungwa na Prince Dube dakika ya 58, limeipa Yanga alama tatu muhimu katika mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi AS FAR Rabat.

Ushindi huo wa bao 1-0, walioupata Wanajangwani hao kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar unaifanya timu kuingia katika mchezo wa pili na matumaini ya kuendelea kufanya vizuri.

Yanga inayonolewa na kocha raia wa Ureno, Pedro Goncalves, itacheza mechi ya pili ya michuano hiyo ugenini Ijumaa ijayo dhidi ya JS Kabylie ya nchini Algeria.

Katika hatua nyingine mshambuliaji wa Yanga, Clement Mzize amepokea tuzo yake ya bao bora Afrika mwaka 2025 iliyotolewa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Novemba 19,2025 nchini Morocco.

Mzize alishindwa kwenda Morocco kuhudhuria halfa ya utoaji tuzo hizo kutokana na hali yake ya kiafya.

spot_img

Latest articles

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...

Waziri Ndejembi atoa maelekezo mazito utekelezaji wa mradi Malagarasi MW 49.6 KIGOMA

📌Hajaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mkandarasi kwenye mradi 📌Aagiza ukaguzi maalum wa matumizi ya...

More like this

DCEA yakamata Lita 66,048 za kemikali bashirifu

NA MWANDISHI WETU MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ((DCEA), imefanikiwa kukamata...

Chevron yaonesha nia ya kuwekeza Tanzania katika sekta ndogo ya Mafuta na Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu KAMPUNI kubwa ya nishati kutoka Marekani, Chevron Corporation imeeleza utayari wake wa...

Jumba la maajabu laiponza Yanga,  yapigwa faini  milioni 30,  Meneja  matatani

Na Mwandishi Wetu KLABU ya Yanga imetozwa faini ya Sh 30 milioni  kwa kosa la...