JKT Queens na matumaini nusu  fainali CAFWCL mbele ya TP Mazembe

Na Mwandishi Wetu

Baada ya timu ya JKT Queens kutoa sare mbili mfululizo Ligi ya Mabingwa Wanawake Afrika (CAFWCL), bado ina matumaini ya kutinga nusu fainali ya michuano hiyo, ambapo mchezo ujao itakutana na TP Mazembe Novemba 15,2025.

Katika michuano hiyo inayoendelea nchini Misri, JKT Queens jana ilitoka sare  ya 1-1 na  Asec Mimosa ya Ivory Coast, mchezo wa kwanza ilitoa suluhu kwanza  dhidi ya  Gaborone United ya Botswana.

Ili kusonga mbele hatua  ya nusu fainali, wawakilishi hao wa Tanzania wanahitaji ushindi mbele ya TP Mazembe ukiwa ni mchezo wao wa mwisho wa kundi B.

Kocha wa timu hiyo, Kessy Abdallah, amewaomba mashabiki wawe na amani kwani, kuelekea mchezo wa mwisho wanaandaa mpango mkakati kuhakikisha timu inakwenda hatua ya nusu fainali.

Naye mlinzi wa kati wa JKT Queens, Ester Maseke, amesema licha ya timu yake kutoka sare dhidi ya Asec Mimosa ya Ivory Coast na kufikisha alama mbili katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa wanawake, bado wanaamini wana nafasi ya kufanya vizuri na kufuzu hatua ya nusu fainali.

Maseke amesema kikosi cha JKT Queens kimeonyesha uwezo mzuri katika michezo iliyopita na kwamba matokeo ya sare hayamaanishi mwisho wa safari yao kwenye mashindano hayo.

Ameongeza kuwa tuzo ya mchezaji Bora wa mechi aliyopata katika mchezo dhidi ya Asec Mimosa ni matokeo ya ushirikiano mkubwa kati yake na wachezaji wenzake.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...