Nyota JKT Queens aipigia hesabu Asec Mimosa

Na Winfrida Mtoi

Mshambuliaji wa JKT Queens FC, Jamila Rajabu, amesema  amejipanga  kutengeneza  nafasi na kufunga mabao katika mchezo wa pili wa hatua ya makundi dhidi ya Asec Mimosa ya Ivory Coast  kwenye  michuano ya  Ligi ya Mabingwa Afrika inayoendelea katika jiji la Ismailia, Misri.

JKT Queens ambayo ni mwakilishi pekee wa Tanzania na Afrika Mashariki katika michuano hiyo, itaivaa Asec Mimosa kesho Novemba 12, 2025. Mchezo wa kwanza ilikutana Gaborone United na kutoka sare ya bao 1-1.

Jamila amesema katika mchezo uliopita walikuwa na mapungufu katika eneo la mwisho, hali iliyochangia kushindwa kupanda ushindi licha ya kupata nafasi kadhaa za kufunga.

Amesema benchi la ufundi tayari limefanyia kazi mapungufu hayo kwa sasa kikosi kipo katika hali nzuri na wana malengo makubwa ya kuibuka na ushindi katika mchezo huo.

spot_img

Latest articles

“MADEREVA TANESCO KUWENI CHACHU UTOAJI HUDUMA BORA”

📌Watakiwa kutunza vyombo vya usafiri ili kuongeza ufanisi wa huduma 📌TANESCO yanunua vyombo vya usafiri...

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...

CRDB yazindua msimu wa nne wa Zogo Mchongo, yasisitiza elimu ya fedha na matumizi ya teknolojia kukuza uchumi

Na Tatu Mohamed BENKI ya CRDB imezindua rasmi msimu wa nne wa kipindi cha Zogo...

More like this

“MADEREVA TANESCO KUWENI CHACHU UTOAJI HUDUMA BORA”

📌Watakiwa kutunza vyombo vya usafiri ili kuongeza ufanisi wa huduma 📌TANESCO yanunua vyombo vya usafiri...

Sasa itoshe kuvumilia uzembe huu

WIKI iliyopita zilisambaa habari za soko jipya la kisasa la Chuini lililojengwa kwa gharama...