Fountain Gate yatoa kocha bora

Na Mwandishi Wetu

Kocha wa timu ya Fountain Gate,  Mohamed Laizer amechaguliwa kuwa kocha bora wa mwezi Oktoba wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2025/26.

Kwa mujibu wa taarifa ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania, Laizer amewashinda Zedekia Otieno wa Tanzania Prisons na Francis Baraza wa Pamba Jiji alioingia nao fainali katika mchakato huo.

Kocha huyo aliiongoza Fountain Gate katika michezo miwili na kujikusanyia alama saba, ikiwa na jumla ya mabao mawili ya kufunga na hajaruhusu bao na kuisaidia timu kutoka nafasi ya 14 hado sita katika msimamo wa ligi hiyo.


Pia kiungo wa timu hiyo Issa Abushiri, amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Oktoba alitoa mchango katika michezo ya timu yake, akifunga bao moja  ambapo Fountain Gate Ilishinda bao 1-0 dhidi ya Dodoma Jiji na ikashinda bao 1-0 dhidi ya KMC na  sare ya 1-1 dhidi ya Coastal Union.

Wakati huohuo Kamati ya Tuzo za TFF, imemchagua Rishedy Kihedu wa Mbuni FC kuwa Mchezaji Bora wa Mwezi Oktoba wa Ligi Championship ya msimu wa  2025/26, huku Leonard Budeba pia wa Mbuni FC akichaguliwa Kocha Bora wa mwezi huo.

Pia Kamati ya Tuzo imemchagua Meneja wa Uwanja wa Tanzanite Kwaraa, Jackson Mwendwa kuwa Meneja Bora wa Uwanja kwa mwezi Oktoba, kutokana na kufanya vizuri katika meneji-menti ya matukio ya michezo pamoja na masuala yanayohusu miundombinu uwanjani.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...

Bokya amtahadharisha mapema Tyson wa Bongo

Na Winfrida Mtoi Bondia Ismail Khalid maarufu Boyka ametamba kutoa kipigo kikali kwa mpinza wake...

More like this

Dk. Mwigulu: Tutamuenzi kwa vitendo marehemu Jenista

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amesema Serikali itayaendeleza mambo yote mema yaliyofanywa na...

Balozi Bandora kuzikwa kesho makaburi ya Kinondoni

Mwanadiplomasia nguli wa Tanzania, aliyewahi  kuwa Balozi wa Tanzania nchini Nigeria na Mratibu Mkazi...

Serikali yajipanga kuimarisha utumishi wa umma, kuendeleza mageuzi ya kidigitali

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa...