Jeuri ya ushindi CAFCL Simba waanza ‘kuchonga’

Na Winfrida Mtoi

Ushindi wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nsingizini Hotspurs katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, klabu ya Simba imetamba kuwa ni kati ya timu tatu Afrika zenye uhakika wa kucheza hatua ya makundi ya michuano hiyo.

Kauli hiyo imetolewa leo Oktoba 21,2025 na Ofisa Habari wa klabu hiyo, Ahmed Ally wakati akizungumza na waandishi kuelekea mchezo wao wa marudiano na  Nsingizini inayotokea Eswatini,  wakisaka tiketi ya kutinga hatua ya makundi. Mechi hiyo itachezwa Jumapili hii Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Ameeleza kuwa wana sababu zote za kuonyesha utofauti kwa kuwa ndiyo timu pekee kutoka Tanzania iliyopata ushindi ugenini katika michezo ya mkondo wa kwanza raundi ya pili Ligi ya Mabingwa Afrika. “Afrika hii timu zenye uhakika wa kucheza makundi mara saba mfululizo ni Al Ahly na Mamelodi na sisi tunaongezeka hapo.

“Tulikuwa tunapiga kelele kwamba Simba yetu hatuelewi inavyocheza lakini sasa imerejea. Simba ya kutisha imerejea, Simba ya kushambulia muda wote imerejea sasa unabaki nyumbani kufanya nini. Na haya sio maneno ya kutoka usingizi, haya ni maneno ya kuona inacheza na pale mwalimu anasema uwanja ulikuwa mdogo. Sasa uwanja wa Mkapa anakwenda kwenye uwanja mkubwa, njoo Uwanja wa Mkapa uone Simba ikifanya balaa zito, amejinasibu Ahmed.

Amesema mchezo huo pia itakuwa ni nafasi pekee kwa mashabiki kuona  uhalisia wa kocha wao mpya  Dimitar Pantev ambaye licha ya ushindi lakini alisema bado hajaridhishwa na kiwango cha timu yake.

spot_img

Latest articles

TCAA YAIMARISHA HUDUMA KWA WATEJA KUPITIA DAWATI MAALUM

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kupitia kwa Mkurugenzi wake...

TBA YASHINDA TUZO YA BANDA BORA SABASABA, YATANGAZA DIRA YA KUFIKIA VIWANGO VYA KIMATAIFA

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umeibuka mshindi wa pili na kutunukiwa tuzo...

VETA yajivunia ushindi, yaeleza mchango wa Mafunzo ya Ufundi Stadi

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imesema ushindi...

Twange: Tanesco yazidi kupanua Nishati Safi ya kupikia, kuimarisha usambazaji wa umeme Zanzibar

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Lazaro Twange, amesema Shirika...

More like this

TCAA YAIMARISHA HUDUMA KWA WATEJA KUPITIA DAWATI MAALUM

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kupitia kwa Mkurugenzi wake...

TBA YASHINDA TUZO YA BANDA BORA SABASABA, YATANGAZA DIRA YA KUFIKIA VIWANGO VYA KIMATAIFA

Na Mwandishi Wetu WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) umeibuka mshindi wa pili na kutunukiwa tuzo...

VETA yajivunia ushindi, yaeleza mchango wa Mafunzo ya Ufundi Stadi

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imesema ushindi...