Simbu afichua siri ya ushindi

Na Winfrida Mtoi

Bingwa wa Dunia wa mbio za Marathoni za kilomita 42, ambaye ni Askari wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ), Sajenti Alphonce Simbu, amesema si rahisi kushinda lakini ukijiandaa, kujituma na kufanya juhudi, unafanikiwa.

Simbu ambaye ameshinda medali ya dhahabu katika mashindano yaliyofanyika Tokyo, nchini Japan, amewaslli leo saa 9:13 alfajiri na kupokelewa na watu mbalimbali pamoja na familia yake.

Akizungumza baada ya kuwasili amewataka wanamichezo wa kitanzania hasa riadha, kufanya juhudi na kujiandaa na wasikate tamaa katika kufikia ndoto zao.

“Niwasihi tu wachezaji wa kitanzania kwamba wanaweza na wasikate tamaa kwa sababu ukikata tamaa unaweza usifikie ndoto zako. Niwaambie tu juhudi, kujituma na nidhamu zinasaidia,” amesema Simbu.

Simbu aliibuka mshindi akitumia muda wa 2:09:48, akiwashinda wanariadha 89 kutoka nchi mbalimbali.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...