Simbu afichua siri ya ushindi

Na Winfrida Mtoi

Bingwa wa Dunia wa mbio za Marathoni za kilomita 42, ambaye ni Askari wa Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ), Sajenti Alphonce Simbu, amesema si rahisi kushinda lakini ukijiandaa, kujituma na kufanya juhudi, unafanikiwa.

Simbu ambaye ameshinda medali ya dhahabu katika mashindano yaliyofanyika Tokyo, nchini Japan, amewaslli leo saa 9:13 alfajiri na kupokelewa na watu mbalimbali pamoja na familia yake.

Akizungumza baada ya kuwasili amewataka wanamichezo wa kitanzania hasa riadha, kufanya juhudi na kujiandaa na wasikate tamaa katika kufikia ndoto zao.

“Niwasihi tu wachezaji wa kitanzania kwamba wanaweza na wasikate tamaa kwa sababu ukikata tamaa unaweza usifikie ndoto zako. Niwaambie tu juhudi, kujituma na nidhamu zinasaidia,” amesema Simbu.

Simbu aliibuka mshindi akitumia muda wa 2:09:48, akiwashinda wanariadha 89 kutoka nchi mbalimbali.

spot_img

Latest articles

IAEA yaipongeza Zanzibar kwa Ushirikiano Katika Kilimo na Mifugo

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Suleiman Masoud Makame,...

Wakurugenzi Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa kwa siku tano

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) kwa kushirikiana na Taasisi ya...

Mkurugenzi Mkuu NIRC atoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali Iringa

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa,...

Baraza la wafanyakazi Siri ya utendaji bora

Na Mwandishi Wetu BARAZA la Wafanyakazi la Sita la TMDA limefanyika kwa ufanisi tarehe...

More like this

IAEA yaipongeza Zanzibar kwa Ushirikiano Katika Kilimo na Mifugo

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar, Suleiman Masoud Makame,...

Wakurugenzi Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa kwa siku tano

Na Mwandishi Wetu OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) kwa kushirikiana na Taasisi ya...

Mkurugenzi Mkuu NIRC atoa pole kwa waandishi wa habari waliopata ajali Iringa

Na Mwandishi Wetu MKURUGENZI Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Raymond Mndolwa,...