Baraza ataja mbinu za kuimaliza Yanga

Na Winfrida Mtoi

Kocha Mkuu wa timu ya Pamba Jiji, Francis Baraza amesema hana presha yoyote kuelekea mchezo wao wa  kesho dhidi ya Yanga  kutokana na alivyojipanga, akijivunia mbinu zake.

Amesema anaamini ana wachezaji wazuri wanaoweza kutoa ushindani kwa Yanga, hivyo ataingia uwanjani kuonesha burudani ya soka  kwa kushambulia na si kwenda kuzuia ‘kupaki basi’  kama wengi wanavyotarajia.

“Mifumo yote mimi nitaipiga, mshakuwa na ile kuwa tutapoteza lakini dakika 90 zitaongea. Najua Yanga ni mabingwa, ni timu imechukua mara nne. Ila mimi sina presha, nikiweka presha nitawaumiza wachezaji wangu,” amesema Baraza.

Kocha huyo raia wa Kenya, amesema kwa kawaida anapokutana na timu kubwa huwa anatumia nafasi hiyo kuwapa fursa wachezaji wake hasa wadogo ili kuonesha uwezo wao na kuthibisha hilo kesho atamuanzisha kijana wa umri chini ya miaka 20 (U -20).

Ameeleza kuwa pamoja na kuwa nchini Kenya lakini anafuatilia Ligi ya Tanzania, msimu mzima uliopita ameifuatilia mechi za Pamba na anajua ni sehemu gani ina shida anaendelea kurekebisha.

 Yanga na Pamba zitakutana katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam, ikiwa ni  mechi ya kwanza ya msimu mpya  kwa Yanga ambayo ni bingwa mtetezi na mchezo wa pili wa Pamba.

spot_img

Latest articles

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...

Wabunge walifuata mkumbo kwenda Morocco kuishangilia Serengeti Boys lawakuta jambo

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Mbunge la Tanzania, Mussa Azzan Zungu ametoa siku nne za...

More like this

Mchezo wa kuogelea wazidi kupaa nchini, TSA  yafichua siri

Na Winfrida  Mtoi MCHEZO wa kuogelea umezidi kushika kasi nchini  kutokana na kuongezeka idadi ya...

Dkt Nchimbi atembelea banda la Tanesco

Na Mwandishi Wetu MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Balozi...

Waogeleaji chipukizi 400 kutikisa Dar kesho

Na Mwandishi Wetu Zaidi ya waogeleaji 400 wenye umri wa miaka 6 hadi 12 wanatarajiwa...