Tembo Warriors yatinga nusu fainali CECAAF

Na Mwandishi Wetu

Timu ya Taifa ya watu wenye ulemavu Tanzania ‘Tembo Warriors’ imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya mashindano ya Afrika Mashariki na Kati (CECAAF) baada ya leo kuichapa Uganda mabao 4-1 katika michuano hiyo inayoendelea nchini Burundi.

Akizungumzia matokeo hayo, Kocha wa Tembo Warriors Ivo Mapunda, amesema ushindi huo umetokana na marekebisho ya kiufundi waliyofanya baada ya kupoteza mchezo uliopita dhidi ya Kenya.

Amesema ilikuwa ni mechi ngumu lakini walipambana kwa sababu ilikuwa ni lazima washinde ili kuendelea na hatua nyingine ya mashindano.

” Leo ilikuwa ni lazima tushinde, nawashukuru wachezaji kwa kufuata maelekezo vizuri, tunachoangalia kwa sasa ni mchezo wetu wa kesho na Burundi ambao ni lazima tushinde ili tuingie fainali,” amesema Mapunda.

Mchezo wa kwanza timu hiyo ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-0 na Kenya ambayo ndiyo inayoongoza kundi B ikiwa na pointi sita, Tanzania ya pili na alama tatu.

spot_img

Latest articles

DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2 YAKAMATWA IKITOROSHWA

Na Mwandishi Wetu KUFUATIA kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini...

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

SAMIA AONGOZA TAIFA KUWAKUMBUKA MASHUJAA WALIOJITOA KWA AJILI YA TANZANIA

Na Mwandishi Wetu MAMIA ya wananchi, viongozi wa Serikali na wakuu wa vyombo vya...

e-GA YASIFU MAGEUZI YA TANESCO KATIKA UTOAJI HUDUMA KIDIGITALI

📌 Wavutiwa namna TANESCO inavyotumia teknolojia na mitandao ya kijamii kutoa huduma nzuri kwa...

More like this

DHAHABU YENYE THAMANI YA ZAIDI YA BILIONI 1.2 YAKAMATWA IKITOROSHWA

Na Mwandishi Wetu KUFUATIA kuimarishwa kwa mfumo wa udhibiti wa biashara haramu ya madini...

Taasisi za Umma zatakiwa kutokuwa kikwazo kwa wawekezaji

Na Mwandishi Pwani SERIKALI imezitaka Taasisi za Umma kuhakikisha zinakuwa chachu ya ukuaji wa uchumi...

SAMIA AONGOZA TAIFA KUWAKUMBUKA MASHUJAA WALIOJITOA KWA AJILI YA TANZANIA

Na Mwandishi Wetu MAMIA ya wananchi, viongozi wa Serikali na wakuu wa vyombo vya...