Serikali yasitisha mchakato uchaguzi TOC

Na Mwandishi Wetu

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imesitisha mchakato wa uchaguzi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), uliopangwa kufanyika Oktoba 4, 2025 baada ya kubainika kutumia Katiba isiyo halali.

Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo leo Septemba 9,2025, imetaja sababu ya kusitishwa kwa mchakato wa uchaguzi huo ni kutokana na kukiukwa kwa taratibu, hivyo kutakiwa kuanza upya.

Taarifa hiyo imesema uamuzi huo wa kusitisha mchakato wa uchaguzi umetolewa na Waziri Pro. Palamagamba Kabudi, akiitaka TOC kuanza upya kwa kutumia Katiba inayotambulika na kisheria na Baraza la Michezo la Taifa (BMT), iliyoidhinishwa Novemba 26, 2020.

“Wizara imechukua hatua hiyo kwa kuzingatia misingi ya demokrasia, uwajibikaji, utawala bora na utulivu katika sekta ya michezo,” imesema.

Aidha, Wizara imesisitiza kuwa rufaa iliyowasilishwa na uongozi wa TOC kuhusu zuio la awali la Msajili wa Vyama vya Michezo, ilikataliwa, na hivyo ni lazima kufuata maelekezo ya Serikali.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...