Serikali yasitisha mchakato uchaguzi TOC

Na Mwandishi Wetu

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imesitisha mchakato wa uchaguzi wa Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC), uliopangwa kufanyika Oktoba 4, 2025 baada ya kubainika kutumia Katiba isiyo halali.

Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo leo Septemba 9,2025, imetaja sababu ya kusitishwa kwa mchakato wa uchaguzi huo ni kutokana na kukiukwa kwa taratibu, hivyo kutakiwa kuanza upya.

Taarifa hiyo imesema uamuzi huo wa kusitisha mchakato wa uchaguzi umetolewa na Waziri Pro. Palamagamba Kabudi, akiitaka TOC kuanza upya kwa kutumia Katiba inayotambulika na kisheria na Baraza la Michezo la Taifa (BMT), iliyoidhinishwa Novemba 26, 2020.

“Wizara imechukua hatua hiyo kwa kuzingatia misingi ya demokrasia, uwajibikaji, utawala bora na utulivu katika sekta ya michezo,” imesema.

Aidha, Wizara imesisitiza kuwa rufaa iliyowasilishwa na uongozi wa TOC kuhusu zuio la awali la Msajili wa Vyama vya Michezo, ilikataliwa, na hivyo ni lazima kufuata maelekezo ya Serikali.

spot_img

Latest articles

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

Msajili wa Hazina, Fitch Ratings watathmini mageuzi ya taasisi za umma

Na Mwandishi wa OTR OFISI ya Msajili wa Hazina (OTR) Jumanne, Agosti 11, 2026, ilifanya...

More like this

RAIS SAMIA KUZINDUA RASMI MRADI WA JNHPP AGOSTI 22, 2026

📌Waziri Ndejembi asema ni tukio la kihistoria litakaloshuhudiwa na watanzania pamoja na wageni 📌Asema...

JAJI MSHIBE ASISITIZA MAANDALIZI YA KISEKTA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA EL NIÑO

Na Mwandishi Wetu MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...