Ivo Mapunda aomba sapoti kwa watanzania CECAAF

Na Mwandishi Wetu

Kocha wa timu ya Taifa ya soka kwa watu wenye Ulemavu Tanzania ‘Tembo Warriors’, ameomba sapoti kutoka kwa Watanzania kuhakikisha wanafanikiwa kutwaa ubingwa wa michuano ya Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAAF), inayofanyika nchini Burundi.

Tembo Warriors ambayo tayari imewasili nchini humo, inatarajia kurusha karata yake ya kwanza kesho September 9, 2025 dhidi ya Kenya.

Mapunda amesema wamejiandaa kufanya vizuri katika mashindano hayo, huku akiwataka watanzania waliopo nchini Burundi kujitokeza uwanjani kusapoti timu hiyo katika  kupambania ubingwa wa mashindano hayo.

“Kwa Asilimia 95% tuko tayari kwa ajili ya mchezo kikubwa tunaomba sapoti ya watanzania waliopo nchini Burundi kuja uwanjani na watanzania waliopo Tanzania kwa dua ili turudi na ubingwa, “amesema Mapunda.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...