Geofrey Timothy achukua fomu ya kugombea Ubunge Jimbo la Kawe

Na Mwandishi Wetu

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Kawe kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Geofrey Timothy, amechukua fomu ya kuwania nafasi hiyo na kuahidi kuwatumikia wananchi wa Kawe kwa ari na moyo wa kujituma.

Akizungumza leo Agosti 26, 2025 mara baada ya kuchukua fomu, Timothy ameishukuru CCM kwa imani waliyoonesha kwake kwa kumteua kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa mwaka huu.

“Nashukuru viongozi wa Chama kwa kuniteua kupeperusha bendera ya chama kupitia Jimbo la Kawe. Yapo mengi tumepanga kuyafanya…nawashukuru wajumbe kwa kunipigia kura nyingi kupeperusha bendera ya chama,” amesema.

Aidha, Timothy amewataka wakazi wa Kawe kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa kampeni za CCM utakaofanyika Agosti 28, 2025, akisema utakuwa ni fursa ya wananchi kusikia kwa kina mipango ya chama na kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan.

Amesema Chama hicho kimejipanga kwa mikakati thabiti ya kuendeleza utekelezaji wa Ilani kwa vitendo, ikiwemo kuboresha huduma za kijamii, kuongeza ajira kwa vijana pamoja na kukuza fursa za kiuchumi.

spot_img

Latest articles

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...

DCEA yakamata Tani 9.93 za Dawa za Kulevya, Watuhumiwa 151 Watiwa Mbaroni

Na Tatu Mohamed  MAMLAKA ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imekamata tani...

More like this

Waziri Gwajima aipongeza Tanesco kuandaa kongamano la wanawake la Nishati Safi ya kupikia

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima...

Makofi, vigelegele vimemrarua Mwigulu Nchemba?

Na Jesse Kwayu KATIKA mfumo wa utawala ambao chimbuko la madaraka ya dola ni wananchi,...

Katibu Mkuu Uwekezaji afanya ziara Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu KATIBU Mkuu wa Ofisi ya Rais – Uwekezaji, Dk. Fred Msemwa, leo...