Chadema yaipeleka Yanga FIFA

Na Mwandishi Wetu

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetuma barua ya malalamiko kwa Shirikisho la Soka la Kimataifa(FIFA), ikilitaka kuifanyia uchunguzi klabu ya Yanga kuhusu kujihusisha na masuala ya kisiasa.

Malalamiko ya Chadema yametokana na Yanga kushiriki katika harambee ya kuchangia fedha za kufanikisha kampeni ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu Oktoba 29,2025 iliyofanyika Agosti 12, 2025, ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam ambapo klabu hiyo ilichangia sh 100 milioni.

Kupitia barua hiyo, Chadema pia imeomba kuchukuliwa hatua za kinidhamu kulingana na Kanuni kwa maofisa na viongozi wa klabu hiyo waliohusika katika jambo hilo la uchangiaji kwa madai kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa kanuni na sheria za FIFA.

“Sisi, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwa heshima tunawasilisha malalamiko rasmi na ombi kuhusu mwenendo wa Young African Sports Club (“Yanga”) ya Tanzania, ambapo vitendo vya hivi karibuni ni ukiukaji wa moja kwa moja wa misingi ya FIFA,”

Mkurugenzi wa Mkurugenzi wa Masuala ya Nje na Diaspora wa Chadema, John Kitoka amethibitisha kuandika barua hiyo na kusema tayari imepokelewa FIFA.

Hivi karibuni baada ya kuibuka mjadala juu ya Yanga kuchangia CCM kwa sababu mashaki wake wana itikadi za vyama tofauti tofauti, uongozi wa klabu hiyo ulitoa taarifa ya ufafanuzi kuwa fedha zilizotolewa katika uchangiaji huo zimetoka Taasisi ya GSM Foundation na sio za mfuko wa wanachama.

spot_img

Latest articles

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...

Dkt. Jafar Seif: Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu Sabasaba larahisisha upatikanaji wa huduma kwa wananchi

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za...

More like this

JAB yazindua mwongozo wa kisheria wa utoaji wa Ithibati ya maisha kwa waandishi

Na Mwandishi Wetu BODI ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa...

BRELA YAIBUA FURSA MPYA ULINZI WA ALAMA ZA BIASHARA KWA WAJASIRIAMALI

Na Mwandishi Wetu Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imewataka wajasiriamali wanaoshiriki...

TTB yakutanisha wadau kujadili mustakabali wa Destination Tanzania

Na Mwandishi Wetu Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) imewakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya...