Chadema yaipeleka Yanga FIFA

Na Mwandishi Wetu

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetuma barua ya malalamiko kwa Shirikisho la Soka la Kimataifa(FIFA), ikilitaka kuifanyia uchunguzi klabu ya Yanga kuhusu kujihusisha na masuala ya kisiasa.

Malalamiko ya Chadema yametokana na Yanga kushiriki katika harambee ya kuchangia fedha za kufanikisha kampeni ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu Oktoba 29,2025 iliyofanyika Agosti 12, 2025, ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam ambapo klabu hiyo ilichangia sh 100 milioni.

Kupitia barua hiyo, Chadema pia imeomba kuchukuliwa hatua za kinidhamu kulingana na Kanuni kwa maofisa na viongozi wa klabu hiyo waliohusika katika jambo hilo la uchangiaji kwa madai kuwa ni ukiukwaji mkubwa wa kanuni na sheria za FIFA.

“Sisi, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwa heshima tunawasilisha malalamiko rasmi na ombi kuhusu mwenendo wa Young African Sports Club (“Yanga”) ya Tanzania, ambapo vitendo vya hivi karibuni ni ukiukaji wa moja kwa moja wa misingi ya FIFA,”

Mkurugenzi wa Mkurugenzi wa Masuala ya Nje na Diaspora wa Chadema, John Kitoka amethibitisha kuandika barua hiyo na kusema tayari imepokelewa FIFA.

Hivi karibuni baada ya kuibuka mjadala juu ya Yanga kuchangia CCM kwa sababu mashaki wake wana itikadi za vyama tofauti tofauti, uongozi wa klabu hiyo ulitoa taarifa ya ufafanuzi kuwa fedha zilizotolewa katika uchangiaji huo zimetoka Taasisi ya GSM Foundation na sio za mfuko wa wanachama.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...