Yanga yapelekwa Angola, Simba Botswana

Na Winfrida Mtoi

Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga itaanza hatua ya awali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Wiliete Benguela ya Angola wakati Simba itacheza na Gaborone United ya Botswana.

Wababe hao wa Tanzania Bara wote wataanzia ugenini kati ya Septemba 19 na 21, 2025 na kurudiana kati ya Septemba 26 na 28, 2025 jijini Dar es Salaam.

Yanga ikipita hatua hiyo itakutana na mshindi wa mchezo kati ya Algeci Plus ya Madagascar dhidi ya Silver Strikers ya Malawi, huki Simba ikivuka hatua itacheza na mshindi wa mchezo wa Bhora ya Zimbabwe na Nsingizia Hotspurs ya Eswatin.

Wawakilishi wa Zanzibar katika Ligi ya Mabingwa Afrika, timu ya Mlandege itaanzia ugenini ikicheza na Insurence ya Ethiopia.

Kwa upande wa Kombe la Shirikisho Azam FC itaanzia nyumbani dhidi ya El Merrekh Bantiu ya Sudan Kusini, Singida Bs wamepangwa kucheza na Rayon Sports ya Rwanda, wakati KMKM ya Zanzibar itacheza na AS Port ya Djibouti ambapo zote zitaanzia ugenini.

Droo ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho imefanyika leo Agosti 9, 2025 jijini Dar es Salaam na kushudiwa na viongozi mbalimbali wa soka hapa nchini na Afrika.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...