Mbaroni kwa kumuua mama mkwe na kumjeruhi mkewe

Na Mwandishi Wetu

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara linamshikilia Jumanne Kibagi, mkazi wa kijiji cha Nyarufu wilayani Bunda kwa tuhuma za kumuua mama mkwe wake  iatwaye  Kabula Masanja (50) na kumjeruhi mkewe  Nyangeta Kunyaranyara (21) kwa kutumia panga.

Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara, tukio hilo limetokea Julai 19, 2025  majira ya saa  7;30 usiku katika kijiji cha Chumwi kilichopo wilayani Musoma, ambapo chanzo kimetajwa kuwa ni mgogoro wa kifamilia kati ya mtuhumiwa na mke wake.

Inadaiwa kuwa  Nyangeta ambaye ni mke wa mtuhumiwa alikuwa akimtuhumu mume wake kujihusisha na  vitendo vya kihalifu hususani wizi hali iliyosababisha mwanamke huyo kukimbilia nyumbani kwa mama yake ambapo mtuhumiwa aliwafuata huko  na kuwashambulia kwa kuwakata mapanga sehemu mbalimbali.

“Majirani walifanya jitihada za kuwapeleka katika kituo cha afya Murangi kwa  jailli ya kupatiwa matibabu ambapo Kabula Masanja alifariki akiwa anaendelea na matibabu,” imesema taarifa hiyo.

Akizungumzia tukio hilo, mke wa mtuhumiwa, Nyangeta, akiwa katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere alikolazwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu ameeleza kuwa mtuhumiwa alifika nyumbani kwao usiku na kutekeleza tukio hilo.

Amesema Jumanne alikuwa mume wake ambaye waliishi pamoja kwa muda wa mwaka mmoja, na waliachana baada ya kugundua mwanaume huyo anajihusisha na matukio ya kihalifu.

Nyangeta amesema kabla ya tukio hilo, Jumanne alimpigia simu mama yake akimjulisha nia ya kwenda kumchukua mke wake (Nyangeta), ambapo mama yake alikataa, na ndipo siku ya tukio alipovamia na kuwakata panga yeye na mama yake.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...