Kenya yajiondoa  mashindano ya  CECAFA 

Na Mwandishi Wetu

Timu ya Taifa ya Kenya ‘Harambee Stars’ imejiondoa katika mashindano maalumu ya CECAFA  yaliyopangwa kuanza leo Julai 21,2025 jijini Arusha  kwa ajili  ya maandalizi ya   michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN- 2024).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirikisho la  Soka nchini Kenya (FKF), uamuzi huo umefanyika kutokana na  mapendekezo na ushauri wa benchi la ufundi la timu hiyo, likiongozwa na Kocha Mkuu Benni McCarthy, baada ya tathmini ya kina ya hali iliyopo kwa sasa, ikiwamo kutoridhishwa na mazingira.

Kenya ilikuwa icheze leo dhidi ya Uganda lakini baada ya kujitoa, itarejea nchini Kenya na kuendelea na maandalizi ya CHAN.

Mashindano hayo maalum yalikuwa yashirikishe  nchi nne za Tanzania, Uganda, Senegal na Kenya.

Michuano ya CHAN inatarajiwa kuanza  Agosti 2, 2025 ambapo Tanzania itafungua   dimba dhidi ya Burkina Faso kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam. 

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...