Tyson wa Bongo afunga mtaa 

Na  Winfrida  Mtoi

Bondia wa ngumi za kulipwa Hassan Ndonga maarufu Tyson wa Bongo amefunga  Mtaa wa Banda Mabibo, Dar es Salaam kutokana na wingi wa mashabiki waliojitokeza kumsapoti katika maandalizi ya pambano lake la  Dar Boxing Derby  dhidi ya Mohammed Mpombo  litakalofanyika Julai 26,2025, Viwanja Vya Leaders Club. 

Tyson ambaye anatokea kambi ya Makatuni Pesa, ameweka wazi kuwa hajawahi kufeli katika mapambano yake mengi aliyocheza na kuwahakikishia ushindi mashabiki zake.

“Ukizungumzia K.O huwa inakuja yenyewe ‘automatic, sababu hata ukiangalia mapambano yangu mawili ya mwisho,  la kwanza nilikuwa nacheza raundi nane lakini nikampiga mtu  raundi ya pili, jingine nilicheza Morogoro katika raundi nane nikampiga mpinzani wangu katika raundi ya sita,” ametamba.

Amewaambia mashabiki zake wasisite kujitokeza siku hiyo kwa kuhofia kwani yeye amejipanga  kushinda kutokana na maandalizi anayofanya.

Mmoja wa mashabiki wa bondia huyo,  Hamza. Mohammed, amesema anamkubali bondia wao kwa sababu siku zote hawana kazi mbovu na ameshuhudia hilo mazoezini  na ulingo utasema siku hiyo.

spot_img

Latest articles

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...

TPDC Yahimiza Wananchi Kulinda Miundombinu ya Bomba la Gesi Asilia

Na Mwandishi Wetu SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limeendelea kuwashirikisha wananchi...

More like this

DAWASA yafafanua sababu ya ukosefu wa maji maeneo ya Kibaha hadi Kisarawe

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)...

Tanesco yatambuliwa kama sekta wezeshi na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM)

📍Yapokea cheti cha pongezi kwa mchango wake katika kuendeleza elimu jumuishi 📍Utambuzi watolewa katika hafla...

DAWASA yaanza kufunga Pampu zitakazoimarisha huduma ya Maji

Na Mwandishi Wetu MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA),...