Ewura CCC: Wananchi wadai fidia wanapocheleweshewa kuunganishiwa maji kwa siku saba za kazi

Na Tatu Mohamed

BARAZA la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura CCC) limesema kuwa wananchi wana haki ya kudai fidia wanapocheleweshewa kuunganishiwa maji kwa siku saba za kazi baada ya kulipia.

Hayo yamebainishwa jana jijini Dar es Salaam na Mjumbe wa Kamati ya Watumiaji kutoka Wilaya ya Ubungo, Jane Joseph, katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).

“Kwa mujibu wa Kanuni ya 34(3) ya Kanuni za Ubora wa Huduma za Majisafi na Usafi wa Mazingira za mwaka 2020, mteja ana haki ya kulipwa Sh15,000 endapo hatapata huduma ndani ya siku saba za kazi baada ya malipo. Na kila siku ya ziada, atapaswa kulipwa Sh5,000,” alisema.

Aidha aliwahamasisha wananchi kufika katika banda la Ewura CCC ndani ya Sabasaba ili kujifunza zaidi kuhusu haki zao, namna ya kufuatilia fidia, na kujiepusha na matumizi ya huduma zisizo na ubora unaotakiwa.

Naye Afisa Uelimishaji na Uhamasishaji wa Ewura CCC, Lugiko Lugiko, alibainisha kuwa wananchi wengi hawafahamu haki zao, na hivyo kukosa fidia zinazostahili.

Alisisitiza kuwa mteja anapaswa kuchukua hatua kwa kuandika barua rasmi kwa mtoa huduma akitaja tarehe ya malipo, changamoto iliyojitokeza, pamoja na kuambatanisha ushahidi kama risiti.

“Watu wengi hudhani fidia italetwa bila kuchukua hatua. Tunasisitiza kuwa haki huambatana na wajibu. Lazima ufuate utaratibu wa kisheria ili kulindwa,” aliongeza Lugiko.

Kwa mujibu wa Sheria ya Ewura Sura ya 414, kifungu cha 30, Ewura CCC imepewa mamlaka ya kuwalinda na kuwatetea watumiaji wa huduma, kusambaza taarifa muhimu na kutoa elimu kwa umma ili kuwajengea uwezo wa kudai haki zao.

spot_img

Latest articles

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...

Waangalizi wa Uchaguzi watakiwa kutoingilia mchakato wa Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi wetu, Dodoma WAANGALIZI wa Uchaguzi wa ndani na wa kimataifa wametakiwa kuzingatia sheria...

More like this

Mwanamke ashikiliwa  Polisi kwa  kumuua mume wake na kumfukia ndani ya nyumba yao

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina...

Padre aliyepotea apatikana akiwa hai

Na Mwandishi Wetu Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kumpata Padre Camillus Nikata wa Jimbo...