Dk.Jingu awashauri vijana kujiandaa kwa uzee

Na Mwandishi Wetu

‎Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. John Jingu, ametoa wito mahsusi kwa vijana na jamii kwa ujumla kujiandaa kwa maisha ya uzee kwa kutumia vizuri rasilimali walizonazo. 

“Ni muhimu vijana wawe na mtazamo wa muda mrefu kwa kuwekeza katika familia, mahusiano mema na miradi ya kiuchumi ambayo itawasaidia wanapoingia uzeeni. Ujana ni hatua ya maandalizi ya uzee, tusikimbie wajibu huu,”

Dk. Jingu ameyasema hayo Julai 03, 2025 alipotembelea Makazi ya Wazee cha Bukumbi yaliyopo mkoani Mwanza kwa lengo la kuwajulia hali wazee wanaoishi katika Makazi hayo pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili.

Aidha ameitaka jamii kushiriki kikamilifu katika kuwatunza wazee wao, kuwaheshimu, kuwaangalia na kulinda dhidi ya vitendo vya kikatili.

‎Katika ziara hiyo, Dk. Jingu amehimiza pia wazee kushiriki katika Uchaguzi Mkuu pamoja na fursa mbalimbali za kiuchumi, ikiwemo zile zinazotolewa kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA). 

‎Katika hatua nyingine,ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mahabusu ya watoto jijini Mwanza ambapo ameeleza kuridhishwa na hatua iliyofikiwa kwani mradi huo umefikia asilimia 90 ya utekelezaji. Ujenzi wa mahabusu hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa mapendekezo ya Tume Maalum iliyoundwa ili kuboresha Taasisi za haki jinai nchini hususan zinazohusiana na watoto.

spot_img

Latest articles

Ridhiwani aipa tano Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na...

Dkt. Kazungu: Nishati Safi ya kupikia ni ajenda ya Dunia, Wizara inaitekeleza kwa vitendo

📌Apokea Magari Mawili kutoka Umoja wa Ulaya kwa ajili ya kuanza kampeni ya kutoa...

Wagombea  urais watano TFF wapigwa chini abaki  Karia 

Na Mwandishi Wetu Kamati ya Uchaguzi ya TFF imewang'oa wagombea watano wa nafasi ya Urais...

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora yaweka wazi nafasi yake kwenye Uchaguzi Mkuu

Na Tatu Mohamed TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imesema kuwa ina...

More like this

Ridhiwani aipa tano Ofisi ya Msajili wa Hazina

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na...

Dkt. Kazungu: Nishati Safi ya kupikia ni ajenda ya Dunia, Wizara inaitekeleza kwa vitendo

📌Apokea Magari Mawili kutoka Umoja wa Ulaya kwa ajili ya kuanza kampeni ya kutoa...

Wagombea  urais watano TFF wapigwa chini abaki  Karia 

Na Mwandishi Wetu Kamati ya Uchaguzi ya TFF imewang'oa wagombea watano wa nafasi ya Urais...