TRA yawaalika wananchi Sabasaba kupata elimu ya Kodi na huduma za TIN

Na Tatu Mohamed

MAMLAKA ya Mapato nchini (TRA) imewaita wananchi kutembea banda lao lililopo katika Viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) maarufu kama Sabasaba ili kupata elimu na huduma mbalimbali za kikodi.

Akizungumza na waandishi wa habari katika banda lao lililopo katika Viwanja vya Maonesho hayo ambayo ni ya 49, Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipa Kodi na Mawasiliano wa TRA, Richard Kayombo amesema wameshiriki katika Maonesho hayo kwa ajili ya kuendeleza kutoa elimu ya kodi kwa wadau wanaofika katika viwanja hivyo.

Amefafanua kuwa katika maonesho hayo TRA ina mambo mengi ikiwemo kuwaelekeza watu kuagiza bidhaa pamoja kuwaelekeza bidhaa zenye misamaha ya kodi.

“Tumeona tuje ili kuwaelimsiha wadau mambo mapya na ya zamani kuhusu Chuo cha kodi, vivutio vya kodi, sekta za kilimo pia ukija bandani kwetu utapata huduma ya kupata TIN namba hapa hapa bandani,” amesema Kayombo.

Ameongeza kuwa, watakaotembelea pia wataelekezwa jinsi ya kutoa taarifa kwa wafanyakazi wasio na maadili ili waweze kuchukuliwa hatua.

“Wateja pia tutawaelewesha jinsi ya kuwaripoti wafanyakazi ambao hawana maadili na tunawaelimisha tunachukua hatua gani kwa watu hao ili waweze kufanya kazi kwa maadili,” amesema.

spot_img

Latest articles

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

More like this

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...