TRA yawaalika wananchi Sabasaba kupata elimu ya Kodi na huduma za TIN

Na Tatu Mohamed

MAMLAKA ya Mapato nchini (TRA) imewaita wananchi kutembea banda lao lililopo katika Viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) maarufu kama Sabasaba ili kupata elimu na huduma mbalimbali za kikodi.

Akizungumza na waandishi wa habari katika banda lao lililopo katika Viwanja vya Maonesho hayo ambayo ni ya 49, Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipa Kodi na Mawasiliano wa TRA, Richard Kayombo amesema wameshiriki katika Maonesho hayo kwa ajili ya kuendeleza kutoa elimu ya kodi kwa wadau wanaofika katika viwanja hivyo.

Amefafanua kuwa katika maonesho hayo TRA ina mambo mengi ikiwemo kuwaelekeza watu kuagiza bidhaa pamoja kuwaelekeza bidhaa zenye misamaha ya kodi.

“Tumeona tuje ili kuwaelimsiha wadau mambo mapya na ya zamani kuhusu Chuo cha kodi, vivutio vya kodi, sekta za kilimo pia ukija bandani kwetu utapata huduma ya kupata TIN namba hapa hapa bandani,” amesema Kayombo.

Ameongeza kuwa, watakaotembelea pia wataelekezwa jinsi ya kutoa taarifa kwa wafanyakazi wasio na maadili ili waweze kuchukuliwa hatua.

“Wateja pia tutawaelewesha jinsi ya kuwaripoti wafanyakazi ambao hawana maadili na tunawaelimisha tunachukua hatua gani kwa watu hao ili waweze kufanya kazi kwa maadili,” amesema.

spot_img

Latest articles

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...

Mambo: Demokrasia haijengwi kwa mashinikizo, vitisho

Na Mwandishi Wetu ALIYEKUWA Mgombea wa Bavicha Taifa, Masoud Mambo amesema kuwa demokrasia ya...

More like this

Mwakinyo kuilipia kisasi Taifa Stars dhidi ya Mnigeria kesho, Furahi apania rekodi

Na Winfrida Mtoi BONDIA wa kimataifa wa Tanzania, Hassan Mwakinyo, ameweka bayana kuwa pambano lake...

Serikali kuendelea kuwawezesha vijana kijamii, kiuchumi

Na Tatu Mohamed WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Joel...

Kids Holiday Festival yawavuta mamia ya watoto, CRDB yatumia jukwaa kujenga uelewa wa fedha

Na Mwandishi Wetu BURUDANI na michezo mbalimbali vilitawala Tamasha la Kids Holiday Festival lililowakusanya...