TRA yawaalika wananchi Sabasaba kupata elimu ya Kodi na huduma za TIN

Na Tatu Mohamed

MAMLAKA ya Mapato nchini (TRA) imewaita wananchi kutembea banda lao lililopo katika Viwanja vya Maonesho ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF) maarufu kama Sabasaba ili kupata elimu na huduma mbalimbali za kikodi.

Akizungumza na waandishi wa habari katika banda lao lililopo katika Viwanja vya Maonesho hayo ambayo ni ya 49, Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipa Kodi na Mawasiliano wa TRA, Richard Kayombo amesema wameshiriki katika Maonesho hayo kwa ajili ya kuendeleza kutoa elimu ya kodi kwa wadau wanaofika katika viwanja hivyo.

Amefafanua kuwa katika maonesho hayo TRA ina mambo mengi ikiwemo kuwaelekeza watu kuagiza bidhaa pamoja kuwaelekeza bidhaa zenye misamaha ya kodi.

“Tumeona tuje ili kuwaelimsiha wadau mambo mapya na ya zamani kuhusu Chuo cha kodi, vivutio vya kodi, sekta za kilimo pia ukija bandani kwetu utapata huduma ya kupata TIN namba hapa hapa bandani,” amesema Kayombo.

Ameongeza kuwa, watakaotembelea pia wataelekezwa jinsi ya kutoa taarifa kwa wafanyakazi wasio na maadili ili waweze kuchukuliwa hatua.

“Wateja pia tutawaelewesha jinsi ya kuwaripoti wafanyakazi ambao hawana maadili na tunawaelimisha tunachukua hatua gani kwa watu hao ili waweze kufanya kazi kwa maadili,” amesema.

spot_img

Latest articles

Wafanyakazi wa Majumbani 700 Watunukiwa Vyeti vya Mafunzo ya VETA

Na Tatu Mohamed ZAIDI ya wafanyakazi wa majumbani 700 wamepatiwa mafunzo maalum na kutunukiwa vyeti...

Kada wa CCM, Lameck Nyambara Ajitosa Ubunge Segerea

KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lameck Nyambara amechukua fomu ya kuwania Ubunge Jimbo...

UDOM Yatoa Elimu ya Ulaji Bora Kupunguza Magonjwa Yasiyoambukiza

Na Tatu Mohamed CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimeshiriki Maonesho ya 49 ya Biashara ya...

2020 Vunjo primaries leader to challenge Dr. Kimei again

Enock Koola (35), a staunch member of the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) party...

More like this

Wafanyakazi wa Majumbani 700 Watunukiwa Vyeti vya Mafunzo ya VETA

Na Tatu Mohamed ZAIDI ya wafanyakazi wa majumbani 700 wamepatiwa mafunzo maalum na kutunukiwa vyeti...

Kada wa CCM, Lameck Nyambara Ajitosa Ubunge Segerea

KADA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lameck Nyambara amechukua fomu ya kuwania Ubunge Jimbo...

UDOM Yatoa Elimu ya Ulaji Bora Kupunguza Magonjwa Yasiyoambukiza

Na Tatu Mohamed CHUO Kikuu cha Dodoma (UDOM) kimeshiriki Maonesho ya 49 ya Biashara ya...