Lissu awaambia wafuasi wake wajiandae akitoka ni mchakamchaka

Na Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa Chama Cha  Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amewaambia wasuasi na viongozi wa chama hicho  kuwa wajiandae  kwani  akitoka  ni mchakamchaka.

Lissu amezungumza hayo leo Julai 1, 2025 wakati alipokuwa anawasalimia   wafuasi na viongozi hao waliofika katika  Mahakama ya  Hakimu  Mkazi Kisutu kufuatilia  kesi ya uhaini  inayomkabili kiongozi huyo.

“Jiandaeni hii biashara tunaimaliza siku hizi hizi, nikitoka ni mchakamchaka, nikitoka tuko barabarani, hayo ya yule Jaji mwingine tutajuana nayo,” amesema Lissu  muda mchache baada ya kesi yake kuahirishwa, huku akiwatania wafuasi hao  kwa kusema  “Jamani mie mfungwa,”

Awali akiwa mahakamani hapo,  mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Franko Kiswaga, Lissu aliomba mahakama hiyo kuwa kama upelelezi ama ushahidi haujakamilika basi aachiwe huru kwa sababu mara ya mwisho waliambiwa upelelezi umekamilika na jalada lipo wa DPP.

Amesema  kuwa anaiomba mahakama hiyo isiahirishe kesi kwa sababu hakuna sababu ya msingi, kwani mara ya mwisho waliambiwa upelelezi umekamilika na wangepewa taarifa ya uamuzi.

Lissu alihoji kwamba inamchukua muda gani DPP kusoma faili la kesi hiyo hali ya kuwa yeye ni msomi wa sheria na kama upelelezi ama ushahidi haujakamilika basi aachiwe.

Akizungumzia  maisha yake ya Gerezani kwa sasa   mambo yamekaa vizuri, anapata  huduma za kiroho na pia anakutana na mawakili wake na anafanya mazoezi.

”Baada ya ku-demand hapa kesho yake Mkuu wa Gereza aliniita akaniambia utakaje, Jumapili inayofuata nilipata Padri kwenye selo yangu nikapata huduma ya kiroho.Bwana jela akasema kingine, nikamwambia nataka nifanye mazoezi mahali salama, akasema na hilo limepita kwa sasa nafanya mazoezi uwanjani napata hewa halisi.

“Na mawakili wangu kwa sasa tunakutana kwenye kachumba kamoja hivi, mambo yamekaa vizuri kabisa, lakini sisemi naenda vizuri  ili niendelee kukaa mule gerezani, hapana gerezani sio pazuri,” amesema Lissu.

Kwa upande wa Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga amesema kuwa kutokana na shauri hilo kuwa na maslahi kwa umma ndio maana wameomba ahirisho ili waje kusema kwamba jalada limefikia hatua gani.Pia DPP amefanya jitihada za kutosha kuhusu hiyo licha ya kuwa na majukumu mengi.

Kutokana na mvutano huo kwa kisheria, Hakimu Kiswaga ameahirisha kesi hiyo hadi Julai 15, 2025.

spot_img

Latest articles

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...

Tanesco yazindua ndege nyuki (Drones) kuboresha miundombinu ya umeme nchini

📌Ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati yake kuimarisha huduma kwa wateja kwa kutumia njia...

More like this

 ‘Umimi’ wa viongozi unaua Jumuiya Afrika Mashariki

KATIKATI ya miaka ya 90 wakati mfumo wa vyama vingi unaota mizizi, lilitokea wazo...

Wanafunzi watatu wafariki dunia baada ya kupigwa na radi Dar

Na Mwandishi wetu WANAFUNZI watatu wa Shule ya Msingi Msongola iliyopo eneo la Msongola,...

Serikali yawataka Wakurugenzi kuongeza thamani inayopimika katika uwekezaji wa hisa chache

Na Mwandishi wetu SERIKALI imewataka wakurugenzi wa bodi za kampuni ambazo ina umiliki wa...