Lissu awaambia wafuasi wake wajiandae akitoka ni mchakamchaka

Na Mwandishi Wetu

Mwenyekiti wa Chama Cha  Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu, amewaambia wasuasi na viongozi wa chama hicho  kuwa wajiandae  kwani  akitoka  ni mchakamchaka.

Lissu amezungumza hayo leo Julai 1, 2025 wakati alipokuwa anawasalimia   wafuasi na viongozi hao waliofika katika  Mahakama ya  Hakimu  Mkazi Kisutu kufuatilia  kesi ya uhaini  inayomkabili kiongozi huyo.

“Jiandaeni hii biashara tunaimaliza siku hizi hizi, nikitoka ni mchakamchaka, nikitoka tuko barabarani, hayo ya yule Jaji mwingine tutajuana nayo,” amesema Lissu  muda mchache baada ya kesi yake kuahirishwa, huku akiwatania wafuasi hao  kwa kusema  “Jamani mie mfungwa,”

Awali akiwa mahakamani hapo,  mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Franko Kiswaga, Lissu aliomba mahakama hiyo kuwa kama upelelezi ama ushahidi haujakamilika basi aachiwe huru kwa sababu mara ya mwisho waliambiwa upelelezi umekamilika na jalada lipo wa DPP.

Amesema  kuwa anaiomba mahakama hiyo isiahirishe kesi kwa sababu hakuna sababu ya msingi, kwani mara ya mwisho waliambiwa upelelezi umekamilika na wangepewa taarifa ya uamuzi.

Lissu alihoji kwamba inamchukua muda gani DPP kusoma faili la kesi hiyo hali ya kuwa yeye ni msomi wa sheria na kama upelelezi ama ushahidi haujakamilika basi aachiwe.

Akizungumzia  maisha yake ya Gerezani kwa sasa   mambo yamekaa vizuri, anapata  huduma za kiroho na pia anakutana na mawakili wake na anafanya mazoezi.

”Baada ya ku-demand hapa kesho yake Mkuu wa Gereza aliniita akaniambia utakaje, Jumapili inayofuata nilipata Padri kwenye selo yangu nikapata huduma ya kiroho.Bwana jela akasema kingine, nikamwambia nataka nifanye mazoezi mahali salama, akasema na hilo limepita kwa sasa nafanya mazoezi uwanjani napata hewa halisi.

“Na mawakili wangu kwa sasa tunakutana kwenye kachumba kamoja hivi, mambo yamekaa vizuri kabisa, lakini sisemi naenda vizuri  ili niendelee kukaa mule gerezani, hapana gerezani sio pazuri,” amesema Lissu.

Kwa upande wa Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga amesema kuwa kutokana na shauri hilo kuwa na maslahi kwa umma ndio maana wameomba ahirisho ili waje kusema kwamba jalada limefikia hatua gani.Pia DPP amefanya jitihada za kutosha kuhusu hiyo licha ya kuwa na majukumu mengi.

Kutokana na mvutano huo kwa kisheria, Hakimu Kiswaga ameahirisha kesi hiyo hadi Julai 15, 2025.

spot_img

Latest articles

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...

Mwanasheria Mkuu wa Serikali: Uchaguzi Mkuu wa 2025 ni halali

Na Mwandishi wetu MWANASHERIA Mkuu wa Serikali, Hamza Johari amesema kuwa, Uchaguzi Mkuu wa...

More like this

ELAF yahimiza maridhiano na amani baada ya Uchaguzi Mkuu

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam TAASISI ya Everlasting Legal Aid Foundation (ELAF) imewataka Watanzania...

Taifa Stars ya Gamondi amrejesha Kelvin John

Na Mwandishi Wetu Kaimu Kocha Mkuu wa timu ya Taifa, Taifa Stars Miguel Gamondi amemrudisha...

‘Hali ya huduma ya maji Dar, Pwani ni shwari’

Na Mwandishi Wetu WAKAZI mbalimbali wa Jiji la Dar es Salaam na Mkoa wa...