Wanaume wana haki ya kulindwa- IGP Wambura

Na Mwandishi Wetu

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Camillus Wambura amesema wanaume nchini wana haki ya kulindwa, kusikilizwa na kupewa heshima ambapo wametakiwa kutumia ofisi za Dawati la Jinsia kuripoti ukatili wanaofanyiwa majumbani.

IGP Wambura amesema hayo wakati akifungua Mradi wa Jengo la ofisi za Dawati la Jinsia na Watoto wilayani Tarime, Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya ambapo jengo pamoja na samani zake limegharimu kiasi cha Sh 300 milioni  ikiwa ni  ufadhiri serikali ya Finland.

Aidha, IGP Wambura amewakumbusha wananchi kuwa, serikali kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali imeweza kuweka mikakati madhubuti katika kukabiliana na vitendo vya ukatili wa kijinsia na unyanyasaji dhidi ya watoto ikiwemo makosa ya ukeketaji ili kuhakikisha kuwa wanaojihusisha na vitendo hivyo wanadhibitiwa kwa kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Pia watendaji wa dawati hilo la jinsia wametakiwa kuhakikisha kuwa, wanatoa huduma zenye viwango kwa wateja au wahanga wa matukio ya ukatili wa kijinsia pamoja na kutafuta ufumbuzi wa kukomesha vitendo vya ukatili kwenye jamii.

spot_img

Latest articles

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...

Mwigizaji, msanii wa Bongo Flava wafariki dunia

Na Mwandishi Wetu MSANII wa filamu nchini, Hashim Kambi, amefariki dunia leo alasiri akiwa anapatiwa...

More like this

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...