Sinema mpya yaanza kuelekea mechi ya Dabi kesho, Simba yakacha mkutano wa wanahabari

Na Mwandishi Wetu

Picha iliyotumwa na klabu ya Simba kwenye mitandao yao ya kijamii ni ujumbe tosha baada ya kocha wao Fadlu Davis na nahodha wa kikosi hicho kushindwa kutokea katika mkutano wa wanahabari leo Juni 24, 2025 kuzungumza kwa mujibu wa kanuni kuelekea mchezo wa kesho wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Yanga unaotarajiwa kupigwa Uwanja wa Benjamini Mkapa.

Katika mkutano huo ambao Yanga ndiyo wenyeji, kama ratiba ilivyoonesha kocha wao Hamdi Miloud alifika kwa wakati akiwa na nahodha Dickson Job, wakazingumza na waandishi wa habari.

Picha iliyotumwa na Simba kwenye mitandao yake ya kijamii muda mfupi baada ya kukacha mkutano wa wanahabari.

Baada ya kumaliza ilitakiwa kuwa zamu ya Simba lakini hakuna aliyeonekana ambapo kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania, Karim Boimanda, wahusika hawapatikani kwenye simu.

Kutokana na hali hiyo, Boimanda aliamua kufunga mkutano huo na kuwataka waandishi wa habari waondoke kwa sababu kuna shughuli nyingine zinatakiwa kuendelea kuliko kisubiri watu ambao hawajui nini kimewakuta.

Kocha Mkuu wa Yanga, Hamdi Miloud akizungumza na waandishi wa habari leo kuelekea mchezo dhidi ya Simba kesho ambapo amesema wana nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Msimu 2024/25.

“Kwa mujibu wa ratiba ilitotumwa kwa klabu zote mbili, Simba ambaye ni mgeni katika mchezo huu alipaswa kuwepo hapa saa 5:30 kuanza mkutano, lakini tumefanya jitihada kadhaa bahati mbaya wahusika hawapatikani kwenye simu kwa hiyo tunashindwa kuelewa changamoto ni nini. Taarifa nyingine zitatolewa baadaye,” ameeleza Boimanda.

Ikumbukwe kuwa kumekuwa na matukio mengi tangu mchezo huu ulipotangazwa kuchezwa Machi 8, 2025 ambapo uliahirishwa baada ya Simba kushindwa kufika uwanjani. Ukapangiwa tarehe nyingine Juni 15, Yanga nayo ikazua jambo kwa kutoa masharti ili icheze mchezo hadi kusababisha baadhi ya viongozi wa Bodi ya Ligi kujiuzulu.

spot_img

Latest articles

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...

Serikali yazindua Jukwaa la Vijana, yataja vijana kuwa mhimili Mkuu wa Maendeleo ya Taifa

Na Tatu Mohamed SERIKALI imezindua rasmi jukwaa la kitaifa la vijana lijulikanalo kama ‘Vijana...

More like this

Yacouba atambulishwa Mbeya City

Na Mwandishi Wetu NYOTA wa zamani wa Yanga, raia wa Burkina Faso, Yacouba Songne, ametambulishwa ...

Waziri Ndejembi: Tanzania ina fursa kubwa ya kuendeleza nishati ya Jotoardhi

Na Mwandishi Wetu WAZIRI wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amesema kutokana na uwepo wa vyanzo...

‘Guardians of the Peak’ kuinua utangazaji utalii wa Kilimanjaro kupitia filamu

Na Mwandishi Wetu MRADI wa Guardians of the Peak, unaoingia msimu wake wa pili,...