Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya wanawake, vijana, watu wenye ulemavu, wafanyabiashara wadogo, wakiwemo mamalishe na babalishe, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuwawezesha kukuza mitaji na kuimarisha shughuli zao za kiuchumi.

Hundi hiyo imekabidhiwa leo Jumanne Aprili 21, 2026 na Rais Samia Suluhu Hassan kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Profesa Riziki Shemdoe, kwa niaba ya kundi hilo.

Katika kongamano hilo, Rais Samia pia ametunukiwa Tuzo ya Malkia wa Nishati Safi iliyotolewa na Umoja wa Mamalishe (Umalita), ikiwa ni kutambua mchango wake katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi nchini.

Akizungumza katika kongamano hilo, Rais Samia amesema shughuli za Mama Lishe na Baba Lishe zinapaswa kutambuliwa na kuheshimiwa kutokana na mchango mkubwa wanaoutoa katika maisha ya kila siku ya Watanzania.

“Mtakubaliana nami kwamba shughuli za Mamalishe na Babalishe zinastahili kutambuliwa na kuheshimiwa kwa hadhi inayolingana na mchango wao katika maisha yetu ya kila siku. Yale yaliyosemwa hapa ya kunyanyaswa, ya kusumbuliwa, hayapaswi kufanywa kwa kundi hili,” amesema.

Amesema kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki yatakayowawezesha wafanyabiashara hao wadogo kufanya kazi zao kwa utulivu na usalama, huku akiwataka viongozi wa maeneo mbalimbali kuacha vitendo vya unyanyasaji dhidi yao.

spot_img

Latest articles

Mganga tiba za asili jela miaka 30 kwa kubaka

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Kasulu imemhukumu mshitakiwa Nuru Hamimu Omary (48), mkulima...

DAWASA yawaunganishiwa maji kwa mkopo wakazi wa Kibosha

Na Mwandishi Wetu Wakazi zaidi ya 100 wa Kitongoji cha Kibosha Mji Mpya wamejitokeza kuomba...

Tume uchunguzi wa matukio Oktoba 29 kukabidhi ripoti, watu 63,603 watoa maoni

Na Mwandishi Wetu TUME ya Uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na...

Wadau wahimiza ujenzi wa miundombinu ya mchezo wa kuogelea kuendeleza vipaji

Na Winfrida Mtoi WADAU wa mchezo wa kuogelea nchini, wamefurahishwa na viwango vilivyooneshwa na...

More like this

Mganga tiba za asili jela miaka 30 kwa kubaka

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Kasulu imemhukumu mshitakiwa Nuru Hamimu Omary (48), mkulima...

DAWASA yawaunganishiwa maji kwa mkopo wakazi wa Kibosha

Na Mwandishi Wetu Wakazi zaidi ya 100 wa Kitongoji cha Kibosha Mji Mpya wamejitokeza kuomba...

Tume uchunguzi wa matukio Oktoba 29 kukabidhi ripoti, watu 63,603 watoa maoni

Na Mwandishi Wetu TUME ya Uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na...