Waziri Ndejembi awasilisha bajeti ya 2026/26, kipaumbele umeme wa uhakika nchini

Na Mwandishi Wetu


Waziri wa Nishati, Deogratius Ndejembi, amewasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa mwaka wa fedha 2026/2027, akiainisha vipaumbele katika sekta ndogo ya umeme kuwa ni pamoja na kuhakikisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa ajili ya kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Akisoma hotuba ya bajeti hiyo Aprili 22, 2026, Bungeni Dodoma, Waziri Ndejembi ametaja vipaumbele hivyo kuwa ni pamoja na kuendeleza uzalishaji wa umeme kupitia mitambo tisa katika Kituo cha Kufua Umeme cha Bwawa la Julius Nyerere.

Pia kukamilisha awamu zinazofuata katika mradi wa kuzalisha umeme kwa nguvu ya jua Kishapu baada ya megawati 50 kuunganishwa kwenye gridi ya taifa na utekelezaji wa mradi wa umeme wa Malagarasi, Kigoma unaotarajia kuzalisha Megawati 49.5 za umeme.

Akizungumzia mafanikio yaliyopatikana katika eneo la uzalishaji umeme, Waziri Ndejembi amesema hadi kufikia mwezi Machi 2026, uwezo wa kuzalisha umeme umeongezeka na kufikia jumla ya megawati 4,522.54 kutoka megawati 4,031.71 mwaka2025 ikiwa ni ongezeko la asilimia 12.17

Amesema ongezeko hili limetokana na kukamilika kwa miradi mbalimbali ya umeme, ukiwemo mradi wa kuzalisha umeme kwa nguvu ya jua Kishapu (awamu ya kwanza) unaozalisha jumla ya megawati 50.

Aidha, katika eneo la usafirishaji, amesema hadi kufikia mwezi Machi 2026, urefu wa miundombinu ya kusafirisha umeme nchini ulikuwa umefikia jumla ya kilomita 8,500.38 kutoka kilomita 7,809.67 mwezi Machi 2025.

“Hadi kufikia Machi 2026, urefu wa miundombinu ya kusafirisha umeme nchini ulikuwa umefikia kilomita 8,500.38 ikilinganishwa na kilomita 7,809.67 zilizokuwepo Machi 2025, sawa na ongezeko la asilimia 9,” alisema.

Amesisitiza kuwa Serikali, kupitia TANESCO, imeendelea kuimarisha huduma kwa wateja kwa kuboresha mifumo ya kidijitali, ambapo ilizindua mita janja (smart meters) zinazowezesha umeme ulionunuliwa na mteja kuingia moja kwa moja kwenye mita.

“Hadi kufikia Machi 2026, jumla ya wateja 105,739 walikuwa wameunganishwa na mita janja, na zoezi hilo linaendelea kwa awamu katika maeneo yote ya nchi,” alieleza Mhe. Ndejembi.

Waziri Ndejembi pia amefafanua kuwa kutokana na hatua zilizochukuliwa katika ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji na usambazaji wa umeme, kiwango cha upatikanaji wa umeme nchini kimeongezeka kutoka wastani wa asilimia 78.4 mwaka 2020 hadi kufikia wastani wa asilimia 85.5.

spot_img

Latest articles

Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya...

Mganga tiba za asili jela miaka 30 kwa kubaka

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Kasulu imemhukumu mshitakiwa Nuru Hamimu Omary (48), mkulima...

DAWASA yawaunganishiwa maji kwa mkopo wakazi wa Kibosha

Na Mwandishi Wetu Wakazi zaidi ya 100 wa Kitongoji cha Kibosha Mji Mpya wamejitokeza kuomba...

Tume uchunguzi wa matukio Oktoba 29 kukabidhi ripoti, watu 63,603 watoa maoni

Na Mwandishi Wetu TUME ya Uchunguzi wa matukio ya uvunjifu wa amani yaliyotokea wakati na...

More like this

Rais Samia akabidhi 94.1 bilioni mikopo ya wanawake, vijana

Na Mwandishi Wetu SERIKALI imekabidhi hundi ya shilingi 94.1 bilioni kwa ajili ya mikopo ya...

Mganga tiba za asili jela miaka 30 kwa kubaka

Na Mwandishi Wetu Mahakama ya Wilaya ya Kasulu imemhukumu mshitakiwa Nuru Hamimu Omary (48), mkulima...

DAWASA yawaunganishiwa maji kwa mkopo wakazi wa Kibosha

Na Mwandishi Wetu Wakazi zaidi ya 100 wa Kitongoji cha Kibosha Mji Mpya wamejitokeza kuomba...