Tanesco yashinda Tuzo ya uhifadhi wa Mazingira kupitia Mradi wa JNHPP

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) limekabidhiwa tuzo ya uhifadhi wa mazingira katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Mazingira Kitaifa yaliyofanyika jijini Dodoma leo tarehe 05 Juni, 2025.

Tuzo hiyo imetolewa kutambua mchango wa TANESCO katika kuhifadhi mazingira kupitia utekelezaji wa Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), ambao umeendelea kuzingatia misingi ya utunzaji wa mazingira sambamba na kuchangia kupunguza gesi joto.

Tuzo hiyo ilitolewa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango, na kupokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Lazaro Twange, katika hafla ya kufunga rasmi maadhimisho hayo.

Kupitia ushiriki wake katika maonesho hayo, TANESCO imeendelea kuonesha dhamira ya dhati ya kutekeleza miradi mikubwa ya umeme kwa kuzingatia usalama wa mazingira, ikiwa ni pamoja na JNHPP na mingine inayolenga kuleta manufaa kwa vizazi vya sasa na vijavyo.

spot_img

Latest articles

Dkt. Biteko: Dunia inaiangalia Tanzania na Afrika Mashariki kuwa Kitovu cha Utalii

📌 Atoa maagizo matatu kwa Wizara ya Maliasili 📌 Rais Samia aiweka Tanzania kwenye...

Gugu asisitiza umuhimu wa ushirikiano Kikanda kukabiliana na uhalifu

Na Mwandishi Wetu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,  Ally Gugu, amesisitiza...

Spika Tulia: Serikali Itaendelea Kupambana na Changamoto ya Mikopo kwa Wanafunz

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia...

Makanisa sita ya Gwajima yafungiwa  Mbeya

Na Mwandishi wetu Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limeyafungia matawi sita ya Kanisa la...

More like this

Dkt. Biteko: Dunia inaiangalia Tanzania na Afrika Mashariki kuwa Kitovu cha Utalii

📌 Atoa maagizo matatu kwa Wizara ya Maliasili 📌 Rais Samia aiweka Tanzania kwenye...

Gugu asisitiza umuhimu wa ushirikiano Kikanda kukabiliana na uhalifu

Na Mwandishi Wetu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,  Ally Gugu, amesisitiza...

Spika Tulia: Serikali Itaendelea Kupambana na Changamoto ya Mikopo kwa Wanafunz

Na Mwandishi Wetu SPIKA wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia...