Twange aanza kazi rasmi Tanesco

📌Aomba ushirikiano ili kuhakikisha wananchi wanaendelea kunufaika na umeme wa uhakika.

📌Aahidi Kuendeleza Mazuri yaliyofanyika TANESCO

Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI Mtendaji mpya wa TANESCO, Lazaro Twange ameahidi kuendeleza mazuri yaliyofanywa ndani ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na kuwaomba ushirikiano viongozi na wafanyakazi wa Shirika hilo ili kutimiza azma ya Serikali ya kuhakikisha Watanzania wanapata huduma ya umeme wa uhakika.

Bwana Twange ameyasema hayo Mei 9, 2025 alipowasili rasmi katika ofisi za TANESCO zilizopo Ubungo, jijini Dar es Salaam ambapo alipokelewa Menejimenti ya TANESCO ikiongozwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji (Utafiti, Mipango na Uwekezaji) CPA. Renata
Ndege.

‘’TANESCO imefanya mambo makubwa kwa kipindi cha miaka hii minne. Nawapongeza sana kwa jitihada hizo, nimekuja kuungana nanyi na mimi ni mtumishi mwenzenu. Wananchi wanategemea sana huduma inayotolewa na Shirika hili na nina imani tutashirikiana kuyaendeleza mazuri yaliyofanyika na kuboresha maeneo mbalimbali ili watanzania waendelee kupata umeme’’, amesema Bw. Twange.

Akiongea Kwa niaba ya Menejimenti Naibu Mkurugenzi Mtendaji (Utafiti, Mipango na Uwekezaji) CPA. Renata Ndege amemkaribisha MD Twange na kumuelezea kwa ufupi mikakati mbalimbali inayoendelea kufanywa ndani ya Shirika na kumuahidi kumpatia ushirikiano kutoka kwa Menejimenti na wafanyakazi wote ili kufikia malengo ya Shirika.

Mkurugenzi Mtendaji Twange aliteuliwa kushika nafasi hiyo Mei 6 mwaka huu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kufuatia kifo cha aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo Mha. Gissima Nyamo-Hanga aliyefariki kwenye ajali ya gari na dereva wake Tarehe 13/4/2025.

spot_img

Latest articles

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...

Mwigizaji, msanii wa Bongo Flava wafariki dunia

Na Mwandishi Wetu MSANII wa filamu nchini, Hashim Kambi, amefariki dunia leo alasiri akiwa anapatiwa...

More like this

Tume Jaji Chande imekwepa kututajia aliyekutwa na ngozi ya ng’ombe

NINGALI ninaitafakari ripoti ya Jaji Mohammed Chande ya matukio ya Oktoba 2025 wakati na...

Adaiwa kumuua mtalaka wake kwa panga kisa nguvu za kiume

Na Mwandishi Wetu JESHI la Polisi mkoani Lindi linamshikilia Hassan Athuman Mpogo (46), mvuvi na...

Rais Ruto kuhutubia Bunge Tanzania

Na Mwandishi Wetu RAIS wa Kenya, William Ruto, anatarajiwa kuhutubia Bunge la Tanzania Mei 5,...