Spika wa Bunge ateta na Dk. Mwapinga, amhakikishia ushirikiano

Na Mwandishi Wetu

Spika wa Bunge la Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Dk. Tulia Ackson, amemhakikishia ushirikiano Katibu Mkuu wa Jukwaa la Mabunge ya Nchi Wanachama wa Mkutano wa Kimataifa wa Ukanda wa Maziwa Makuu (FP-ICGLR), Dk. Deo Mwapinga katika utekelezaji wa majukumu yake mapya.

Dk, Tulia ameyasema hayo leo Mei 8, 2025 wakati alipomkaribisha  kufanya mazungumzo na  Dk. Deo Mwapinga, ofisini kwake Bungeni, Dodoma.

Katika mazungumzo hayo, Dk. Tulia amempongeza Dk. Mwapinga kwa kuchaguliwa katika wadhifa huo muhimu wa  kuliongoza Jukwaa hilo na kusisitiza   dhamira ya Tanzania kuendelea kushirikiana na taasisi za kikanda  kukuza demokrasia, utawala bora na maendeleo endelevu.

Dk. Mwapinga alichaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa FP-ICGLR Aprili 25, 2025 katika kikao cha juu cha Maspika wa Mabunge ambayo ni Wanachana wa Jukwaa hilo kilichofanyika Luanda, Angola.

Kwa  mujibu wa Katiba ya Jukwaa hilo ataongoza taasisi hiyo kwa kipindi cha miaka mitatu , ikiwa ni nafasi inayoweza kurejewa.

spot_img

Latest articles

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...

Tanesco Kigamboni yatoa elimu y nishati safi ya kupikia shule ya msingi Malaika

Na Mwandishi Wetu KATIKA kuunga mkono jitihada za Serikali za kuhamasisha matumizi ya nishati...

More like this

Yanga yaikung’uta vibaya Mashujaa FC

Na Winfrida Mtoi WANANCHI Yanga wameichakaza timu ya Mashujaa mabao 6-0, huku nyota mpya wa...

Watumishi wapya wa Ofisi ya Msajili wa Hazina wapigwa msasa

Na Mwandishi Wetu, Pwani OFISI ya Msajili wa Hazina (OMH), kwa kushirikiana na Chuo cha...

Kituo cha kupoza umeme Mtera kuboresha upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Na Mwandishi Wetu SERIKALI kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza...