Serikali kuhakikisha Barabara zote za Halmashauri zinafunguliwa

Na Mwandishi Wetu, Singida

SERIKALI inaendelea kuhakikisha kwamba barabara ambazo zipo katika kila halmashauri ya wilaya zinafunguliwa ili kurahisisha usafiri na usafirishaji katika maeneo ya wananchi.

Hayo yamesemwa na Meneja wa TARURA Mkoa wa Singida Mhandisi Ibrahimu Kibassa kwenye Maonesho ya Usalama na Afya Mahali Pa Kazi katika viwanja vya Mandewa Mkoani Singida.

Mhandisi Kibassa alisema katika mwaka wa fedha wa 2024/2025 TARURA ilipangiwa kutumia Sh.bilioni 886.3 ambazo zimefanikiwa kujenga barabara za kilometa 278.32 za kiwango cha lami na kilometa 9334 za kiwango cha changarawe.

Aliongeza kuwa TARURA imekuwa ikitumia teknolojia ya ujenzi wa madaraja kwa kutumia mawe ambapo yapo madaraja 401 nchini na kwa Mkoa wa Singida yapo madaraja 34 yaliyojengwa kwa mawe na mkoa wa Kigoma unashika nafasi ya kwanza kwa kujenga madaraja mengi ya mawe ikifuatiwa na Arusha.

“Ujenzi wa madaraja kwa teknolojia ya mawe tunatumia sana kwasababu gharama zinapungua kwa asilimia 60 ukilinganisha na teknolojia nyingine za kutumia kokoto kama ilivyo kawaida,” alisema.

Alisema kushuka kwa gharama za ujenzi wa madaraja kwa kutumia mawe kunatokana na kwamba mawe hayo yanapatikana kwenye mazingira ya wananchi ambapo nao wananufaika kwa kipato na hivyo kuinua uchumi wao.

spot_img

Latest articles

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...

Msajili wa Hazina aikaribisha Jeune Afrique Media Group kuangazia fursa za uwekezaji

Na Mwandishi Wetu MSAJILI wa Hazina, Nehemiah Mchechu, amekutana na kufanya mazungumzo na Frederic...

More like this

Dk. Mwigulu ajadiliana na Kamati ya Maandalizi AFCON 2027

Na Mwandishi Wetu WAZIRI Mkuu, Dk. Mwigulu Nchemba amekutana na  Kamati ya Kitaifa ya Maandalizi...

Coastal Union yawatembezea kichapo maafande wa Magereza

Na Mwandishi Wetu TIMU ya Coastal Union imetembeza kichapo cha mabao 4-1 kwa maafande wa...

Simba yazitaka pointi tatu kwa KMC kesho

Na Winfrida Mtoi KOCHA Mkuu wa timu ya Simba, Steve Barker ameweka wazi kuwa hakuna...